• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Baraza la Vyama vya Siasa Laonya na kukemea Wanasiasa wachochezi

Posted on: March 13th, 2025



Baraza la Vyama vya Siasa hapa nchini limewaonya na kukemea vikali tabia ya baadhi ya wanasiasa kutumia vibaya majukwaa ya kampeni za siasa kwa kuhamasisha uchochezi na uvunjifu wa Katiba, Sheria za nchi na ukiukwaji wa maadili ya Kitanzania.

Agizo hilo limetolewa Machi 13, Mwaka huu na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bw. Juma Khatibu, wakati wa kikao cha siku mbili cha Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Nashera. Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kuvipa uwezo vyama vyote 19 vya siasa nchini.

Akifafanua zaidi, Bw. Khatibu amesisitiza kuwa vyama vya siasa vinapaswa kuheshimu Katiba, Sheria za nchi, maadili ya vyama vya siasa, maadili ya uchaguzi na maadili mengine ya kitaifa ili kudumisha amani, utulivu na umoja wa Taifa.

"Baraza la Vyama vya Siasa linakemea vikali wanasiasa wanaotumia vibaya majukwaa ya siasa kuhamasisha uvunjifu wa Katiba, Sheria za nchi na maadili ya Kitanzania," amesema Bw. Juma Khatibu.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo ameviasa vyama vya siasa kuwa na programu maalum za kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za siasa na kushika nafasi za uongozi.

Pia, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa jitihada zake katika kutetea haki za wanawake na kuwapa fursa za kiuchumi, kielimu na uongozi, kwani hatua hizo zinaendelea kuisaidia jamii.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa United Democratic Party (UDP), Bi. Saum Rashid, amewaasa wanasiasa kuandaa mazingira ya amani na utulivu kwa jamii kwa kuepuka mihemko na maneno yanayoweza kuleta mgawanyiko kwani uchaguzi ni chombo cha maendeleo, hivyo wananchi wanapaswa kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo kwa manufaa ya Taifa.

Naye, Katibu Mkuu wa Democratic Party (DP), Bw. Abdul Mluya, amewakumbusha wananchi kwenda kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili kupata fursa ya kushiriki uchaguzi mkuu ili kupata viongozi wenye na maendeleo hapa nchini.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.