• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA WAFANYAKAZI SEKRETARIETI YA MKOA WA MOROGORO LAPITISHA BAJETI 2023/2024.

Posted on: March 10th, 2023


 Viongozi wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya RS Morogoro pamoja na Viongozi wa TUGHE Taifa wakiwa kwenye kikao cha baraza hilo Machi, 9 mwaka huu. Kutoka kushoto ni Mjumbe wa Baraza la TUGHE Taifa  Dr. Mtungilwa, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala Bw. Herman Tesha na  afisa bajeti kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Erick Ulomi. 

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro wamepitisha bajeti kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo takribani 11,873,795,000 zinatarajiwa kutumika kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo.

Bajeti hiyo imepitishwa Machi 9 mwaka huu na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro kwenye ukumbi wa Mikutano uliopo katika Ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Afisa Bajeti Bw. Erick Ulomi akisoma mpango wa bajeti ya Baraza la wafanyakazi Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro kwenye ukumbi wa Mikutano uliopo Ofisi ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akisoma mpango wa bajeti ya Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro mbele ya wajumbe wa kikao hicho Afisa Bajeti kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Bw. Erick Ulomi amesema kati ya fedha hizo shilingi 8,079,813,000 zitaelekezwa kwenye matumizi ya kawaida ambayo yanajumuisha shilingi 3,776,918,809 kwa ajili ya mishahara na shilingi 4,243,316,000 ni matumizi mengineyo.

Aidha, Katika kikao hicho wajumbe wamependekeza suala la ajira  kwa wafanyakazi wapya kwa kada mbalimbali lipewe kipaumbele ili kuziba mapengo  ya watumishi yaliyotokana na kustaafu, kifo na kuhama kwani kasi ya kupungua watumishi kwa kila kada ni kubwa kuliko kasi ya kuajiri na hivyo kuathiri utendaji kazi katika ofisi mbalimbali.

wajumbe wa baraza la wafanyakazi Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro wakiwa kwenye kikao cha kutoa mapendekezo ya bajeti ya 2023l2024.

Sambamba na hilo, wajumbe hao pia wameshauri Mkoa kujenga hoja na kuwasilisha hoja hizo ngazi ya Taifa ili kuongezewa Bajeti ya Mkoa kutokana na ukubwa wa Mkoa ukilinganisha na baadhi ya mikoa mingine pamoja na changamoto nyingine zinazojitokeza ndani  ya Mkoa huo.

Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Bw. Herman Tesha ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya  UTAWALA  aliwataka wajumbe wa kikao hicho kupitia kwa makini wasilisho la bajeti hiyo na kutoa maoni yao ili kuboresha bajeti hiyo kabla ya kuwasilishwa na kuidhinishwa na bunge lå Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Sekretarieti ya Mkoa huo iliidhinishiwa kutumia shilingi 11,873,795,000 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na mmaendeleo, Kati ya fedha hizo shilingi 8,079,813,000 zilitengwa kwa ajili matumizi ya kawaida zilizojumuisha shilingi 3,836,497,000 kwa ajili ya mishahara na shilingi 4,243,316,000 matumizi mengineyo.

Mmoja wa wajumbe wa Baraza hilo akichangia hoja wakati wa kikao hicho

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.