• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

China na Tanzania kufanya kwa pamoja maonesho ya Utalii, Utamaduni.

Posted on: December 5th, 2023

Tanzania na China zinaendeleza udugu wa siku nyingi kwa kupanga kufanyika kwa pamoja maonesho ya Utalii na Utamaduni ili kudumisha ushirikiano zaidi wa nchi hizo mbili kwa faida ya watu wa mataifa hayo.

Hayo yamebainishwa Disemba 5, 2023 na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Chen Mingjian alipofika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima na kufanya mazungumzo yakilenga kudumishi ushirikiano uliokuwepo kwa miaka mingi huku wakigusia ushirikiano zaidi katika sekta za kilimo na utalii.

Balozi Chen Mingjian amesema kuwa China na Tanzania zina uhusiano imara ulioanza tangu marais wa kwanza wa nchi hizo hivyo zimepanga kuendeleza umoja huo kwa uuandaa maonesho ya pamoja ya  Utalii na Utamaduni ifikapo 2024. Lengo likiwa ni kukuza sekta hizo mbili za utalii na utamaduni na Kilimo. 

Amesema, kwa upande wa Sekta ya Kilimo, China itashirikiana na Tanzania kuboresha reli ya TAZARA ambayo ndiyo kitovu kikuu cha njia kuu ya usafirishaji mazao kwa wakulima wa Mkoa wa Morogoro kupeleka Dar es salaam na nchi jirani kama vile Zambia.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemshukuru Balozi huyo kwa ujio wake ndani ya Mkoa wa Morogoro kwani anaamini kuwa Sekta ya Kilimo Mkoani humo inakwenda kukua.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema uwepo wa Reli ya TAZARA itasaidia wakulima wa Mkoa huo kusafirisha mazao yao kwenda sokoni hivyo ameishukuru Serikali ya China kwa kuwa na mpango mahususi wa kuiboresha reli hiyo.

Aidha, Mhe. Malima amemtaka Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na uzalishaji Mali Dkt. Rozalia Rwegasira kushirikiana na Mtaalam wa Mbegu kutoka nchini China ambaye ameanzisha shamba darasa la zao la Soya kuona namna ya kuhamasisha kilimo cha zao hilo kwa wakulima wengine.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewaomba Wataalam hao wa Kilimo kutoka China, kushirikiana na uongozi wa Mkoa ili kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao mbalimbali likiwemo zao la Mkonge ambalo kwa sasa linazalishwa kwa wastani wa tani laki 6.


Ziara ya Balozi huyo wa China Mkoani Morogoro ilikuwa na lengo la kuangalia shughuli za Kilimo katika mashamba darasa yaliyopo vijiji vya Pea pea, Mtego wa Simba wilayani Morogoro na mashamba yaliyoko Mgeta Wilayani Mvomero.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.