• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DC KILAKALA AHIMIZA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KWA NGOs.

Posted on: August 28th, 2024



Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Mussa Kilakala ameyataka mashirika yasiyokuwa ya kiserikali Mkoani Morogoro kufanya kazi kwa uwazi hususan katika kutoa taarifa za utendaji wao ili kuaminiwa na Serikali na jamii kwa ujumla hivyo  kuleta mabadiliko chanya ndani ya jamii.

Ushauri huo umetolewa Agosti 28, 2024 na   Mkuu huyo wa Wilaya akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima   wakati akifungua  jukwaa la mashirika yasiyo ya kiserikali Mkoani humo lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Kiongozi huyo amesema kutokuwa na taarifa sahihi  kunaathiri ufanisi wa usimamizi wa  miradi na kusababisha hasara na upotevu wa rasilimali, hivyo ni jukumu la kila Shirika kutoa raarifa sahihi, kwa uaminifu na kwa wakati kwa maslai mapana ya Taifa.

"...Nasisitiza kuwa ni wajibu wa mashirika kuhakikisha uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa taarifa ili kuleta uaminifu na kuendelea kuleta mabadiliko chanya katika jamii zetu...." amesema Mhe. Kilakala.

Mhe. Kilakala amesisitiza kuwa Mkoa wa Morgoro una julma ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali 499 ambapo 438 kati yake yanafanya kazi na mashirika 61 sawa na 12% yamesimamishwa kufanya kazi zao kwa kutokukidhi vigezo.


 Amesema, mashirika 393 sawa na asilimia 90 ya mashirika yote yaliyohai (438) yanafanya kazi ngazi ya Taifa.

Akifafanua zaidi Mhe. Kilakala amesema, idadi kubwa ya mashirika yanayofanya kazi ngazi ya Taifa yanachangamoto katika utoaji wa taarifa na ufuatiliaji wa shughuli zao huku akinainisha kuwa baadhi ya mashirika hayo huhamisha Ofisi zao kwenda maeneo mengine bila kutoa taarifa, hali inayopelekea ugumu katika ufuatiliaji wa kazi zao.

Hivyo, ameyataka mashirika hayo kutumia  jukwaa hilo kuweka mikakati bora zaidi  na madhubuti ili kuondokana na sifa hizo zinazokiuka masharti ya usajiri wao.


Kwa upande wake Bw. Otanamus Nicholaus Mwenyekiti wa NACONGO Mkoa wa Morogoro amesema lengo la majukwa hayo ni kupeana taarifa, kujua changamoyo zinazoyakabili mashirika na kutoa elimu ya mambo yanayohusu NGOs.


Katika hatua nyingine kiongozi huyo ametoa wito kwa mashirika hayo kufanya kazi zao kwa mujibu usajiri waliopewa, sheria za Nchi na kuwa wazalendo pamoja na kuisaidia jamii.


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utunzaji na Uhifadhi wa Mazingira Bi. Sophia Kalinga amesema mashirika hayo yapo kwa lengo la kuisaidia Serikali katika utoaji wa huduma za kijamii na kuwaletea wananchi maendeleo yao.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.