• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

Posted on: May 23rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema kuwa Serikali ya Mkoa imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa ndani ya miaka miwili, uzalishaji wa maziwa utachangia Shilingi bilioni 18 kwa mwaka katika uchumi wa Mkoa huo, hatua itakayosaidia kukuza uchumi wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.


Mhe. Malima ametoa kauli hiyo Mei 23, Mwaka huu, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu maadhimisho ya wiki ya maziwa kitaifa itakayoanza kufanyika kuanzia Mei 27 hadi Juni 1, Mwaka huu.


Amesema kuwa licha ya Mkoa huo kuwa na idadi kubwa ya ng’ombe, bado hakuna uzalishaji wa maziwa wenye tija. Hata hivyo, tayari Serikali ya Mkoa imeweka mikakati ya kuhakikisha maafisa ugani wanatoa elimu kwa wafugaji ili kufanikisha uzalishaji wa lita 50,000 za maziwa kwa siku.


Kwa sababu hiyo, Mhe. Malima amezitaka taasisi za MORUWASA na RUWASA kupunguza gharama za uchimbaji wa visima ili wafugaji waweze kupata maji kwa urahisi, hatua itakayosaidia mifugo kutosafiri umbali mrefu kutafuta maji.


Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa ameishauri Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) kuendelea kutoa elimu wakati wa wiki ya maziwa kuhusu njia bora za uzalishaji na uhifadhi wa maziwa, ili kuhakikisha maziwa yanayozalishwa yanakuwa yenye ubora na salama kwa matumizi ya binadamu.


Kwa upande wake, Afisa Teknolojia ya Chakula kutoka Bodi ya Maziwa Tanzania, Bw. Rajilan Hilali, amesema Bodi hiyo imeweka mikakati madhubuti ya kuongeza uzalishaji wa maziwa hapa nchini.


Ameongeza kuwa kwa mwaka 2024/2025, uzalishaji wa maziwa umefikia lita bilioni 4.01 kutoka kwa ng’ombe milioni 39 waliopo nchini, ingawa bado kuna changamoto ya uzalishaji kutokana na aina ya mifugo inayofugwa, hasa mifugo ya kienyeji.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.