• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

Posted on: May 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Ali Malima ameutaka uongozi wa Bonde la Wami Ruvu kuhakikisha wanaendelea na taratibu za kubaini vyanzo vya maji ndani ya manispaa ya Morogoro, kuchimba visima  na kupata maji ili kuondoa changamoto ya maji inayowakabili wananchi wa Manispaa hiyo kwa muda mrefu.

Wito huo umetolewa Mei 24, 2025 na Mhe. Malima wakati alipotelembelea maeneo yaliyobainika kuwa ni vyanzo vya maji ambayo ni Maeneo ya Mafisa (Kaenzi) na Kata ya Tungi yaliyopo Halmshauri hiyo.

Mhe. Malima amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Dkt. Samia Suluh Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa mitambo kwa aajili ya kuchimba visima katika kila mkoa, hivyo kupitia kamati ya maji ihakikishe inaendelea na utafiti wa maeneo mengine huku maeneo yaliyobainika kuwa na vyanzo vya maji yaanze kuchimbwa na kusambaza maji kwa wananchi.

"... nimewaelekeza Bonde la Wami Ruvu waendelee kutafuta maji maeneo yale, haya maeneo tunayobaini kama tutapata maji kwa ujumla kama lita milioni 3 kwa siku tutaweza kupunguza adha ya maji.." amesema Mhe. Adam Malima

Kwa upande wake Meneja wa Idara ya Rasilimaji za Maji Bonde la Wami Ruvu Bw. Mrtin Daud Kasambara amesema maeneo yaliyobainika kuwa na vyanzo vya maji ni eneo la Tungi ambapo kisima hicho kinazalisha maji lita zaidi ya 23,000 kwa saa na eneo la mafisa ambapo kisima kitazalisha maji lita 30,000 kwa saa hivyo kusaidiq kupunguza adha ya maji kwa wananchi  wa manispaa ya morogoro.

Naye mwananchi wa Kata ya Tungi Bw. Bululu Wai ameushukuru uongozi wa Mkoa kwa kushirikiana na Idara za maji kuhakikisha wanaondoa changamoyo ya maji katika eneo la Tungi amabapo eneo hilo wananchi wanakumbana na uhaba wa maji.

Imebainika kuwa wajumbe wa Kamati ya maji Mkoani humo ni pamoja na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini  (RUWASA), Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA) Bonde la Wami Ruvu, Maafisa ardhi wa Mkoa na Halmashauri pamoja na wajumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.


MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.