• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DC Kilosa atakiwa kusimamia Amani Ngaite, DED kuunda tume ya kusimamia na kuelekeza wakulima Block Na. 422

Posted on: December 22nd, 2020


Wananchi wa Vijiji vya Ngaite na Tindiga Wilayani Kilosa ambako kuna mgogoro baina ya Jamii ya Wakulima na Wafugaji kugombania ardhi Block Na. 422 iliyoko ndani ya Lanch ya NARCO Mkoani humo, wametakiwa kuendelea kufanya shughuli zao za kilimo na ufugaji ndani ya Block hiyo kwa utaratibu utakaoelekezwa na Kamati itakayoundwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kilosa hadi hapo Serikali itakapotoa maelekezo mengine.

Agizo hilo limetolewa Disemba 22 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare alipofanya ziara ya siku moja katika kijiji cha Ngaite Wilayani Kilosa ili kutatua mgogoro huo ulitaka kuhatarisha amani na utulivu kwa wananchi wa Vijiji vya Ngaite na Tindiga kutokana na kila upande kudai kuwa eneo la Block Na. 422 kuruhusiwa kufanya shughuli za kiuchumi za Ufugaji na Kilimo.

Loata sanare amesema wakati wanasubiri kuoneshwa mipaka na Maafisa kutoka NARCO, amewataka wananchi wa vijiji hivyo kuendelea na kilimo katika mashamba yao ya zamani na kufugia kwenye maeneo ya awali pasipo kuazisha maeneo mapya ya mashamba au Ufugaji.

Katika hatua nyingine, Loata Sanare amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi kupitia Kamati yake ya Ulinzi na Usalama kusimamia Amani na Utulivu wa eneo lenye mgogoro wa ardhi baina ya vijiji viwili vya Tindiga na Ngaite ili wananchi waendelee na shughuli za uzalishaji bila kubughudhiwa lakini bila kukiuka maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa.

“simamieni hilo, amani itokee, ng’ombe kwa mujibu wa viongozi wanasema watakuwa na shida sehemu ya kula lakini tumesema wale hivo mpaka mwafaka utakapotokea" aliagiza Loata Sanare.

Sambamba na agizo hilo Mkuu huyo wa Mkoa, amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale kuunda Kamati huru ya kusimamia na kuhakikisha wakulima hao wanapata maeneo ya kulima pamoja na kulipia maeneo hayo, huku akimuagiza kuwa makusanyo ya fedha zote zinazotokana maeneo hayo kusimamiwa na Ofisi yake.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa NARCO ambaye alihudhuria kikao hicho, kwa niaba ya Meneje Mkuu Ndg. Mnzava Immanuel amekili suala hilo kutokamilika kwa muda uliopangwa na kuahidi zoezi la kuweka  mipaka ya eneo lenye mgogoro kuanza kufanyiwa kazi  mara baada ya sikukuu za Krismas na Mwaka mpya.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake Amina Kibuna ameiomba serikali kuharakisha uwekaji wa mipaka katika maeneo hayo kwa sababu muda wa kuandaa mashamba umefika ili kila mmoja awe huru kufanya shughuli zake kwa utulivu.

 

MWISHO

;


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.