• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2025 IMEWEZESHA TAIFA KUPIGA HATUA ZAIDI.

Posted on: July 17th, 2023

Imeelezwa kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 imeweza kwa kiasi kikubwa kusogeza mbele  maendeleo ya nchi katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, huduma za afya, miundombinu, maji pamoja na maendeleo ya kiuchumi licha ya changamoto mbalimbali ikiwemo Covid 19 ambayo imesababisha kuchelewa kwa baadhi ya mipango.

Hayo yamebainishwa Julai 17 mwaka huu na Mjumbe wa Sekretarieti ya Maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 Dkt. Crispin Ryakitimbo kwenye semina elekezi ya uelimishaji umma ngazi ya Mikoa kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 iliyofanyika  katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Dkt. Crispin Ryakitimbo akitoa wasilisho kuhusu mafanikio ya Dira ya Maendeleo ya 2025 na mchakato wa maandalizi ya Dira ya Maendeleo 2050.

Dkt. Crispin amesema utekelezaji wa Dira ya 2025 umechochea ukuaji wa uchumi wa Taifa kwa zaidi ya 6% kwa mwaka tangu mwaka 2,000 na umewezesha kuongezeka kwa kipato cha mwananchi kufikia wastani wa  sh. 2,844,641 mwaka 2022 kutoka sh. 1,621,445 mwaka 2013 na chini ya shilingi milioni moja mwaka 2,000.

Amesema, Dira hiyo pia imeongeza upatikanaji wa huduma za jamii zikiwemo elimu, afya, maji, uchukuzi, mawasiliano na usafirishaji hususan viwanja vya ndege na bandari na kwamba mafanikio haya yanatokana na uwepo wa dira  inayoongoza katika kufanyia kazi vipaumbele vilivyopo.

Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba akizungumza na wadau wa maendeleo wakati akifungua semina elekezi ya uelimishaji umma kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo.

Akifungua semina hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima amesisitiza Viongozi mbalimbali Mkoani humo walioshiriki kikao hicho kushirikisha wadaumbalimbali kwenye mchakato wa maandalizi ya Dira hiyo ili kupata maoni yatakayo isaidia nchi katika kukua zaidi kiuchumi.

Aidha, ameongeza kuwa dira ya maendeleo ya Taifa ina gusa makundi yote, hivyo anatarajia ushirikishwaji mpana wa wadau wote, ngazi zote zikiwemo taasisi za elimu, sekta binafsi, na asasi za kiraia na mwananchi mmoja mmoja.

Nae, Bi. Senerina Kateule Makamu Mkuu wa chuo cha Taasisi ya elimu ya watu wazima (WAMO)Mkoa wa Morogoro amesema kupitia semina hiyo atahakikisha kuwa anatoa elimu kwa wafanyakazi pamoja na wanafunzi wa Chuo hicho ili waweze kutoa maoni kuhusu Dira ya taifa 2050.

Aidha, Bi. Senerina ameongeza kuwa Dira ya maendeleo 2025 imeisaidia sekta ya elimu kukuwa ikiwemo upatikanaji wa mikopo kwa vyuo vya kati ambayo itawasaidia wanafunzi kujiendeleza kielimu na kuwaondolea wazazi mzigo wa ada kwa watoto wao.

Dira ya Maendeleo 2025 ilianza kutekelezwa mwaka 2000 na utekelezaji wake utakamilika 2025 na kuaza kutekeleza Dira hiyo 2050  huku lengo likiwa ni kuiwezesha nchi kuingia katika kundi la nchi za uchumi wa kati.

Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba (katikati walio kaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa timu ya uandishi wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, viongozi wa Mkoa na Wilaya pamoja na wadau wa Maendeleo baada ya semina elekezi ya uelimishaji umma.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.