• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DKT. JAFO ATAKA KUUNDWA TIMU YA KUFUFUA VIWANDA MOROGORO.

Posted on: July 20th, 2024


Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Seleman Jafo (mb) amemusgiza Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara kuunda timu ya watu nane (8) wakishirikiana na Mkoa, Msajili wa Hazina (TR) ili kuangalia viwanda ambavyo havifanyi vizuri katika Mkoa wa Morogoro na kuona jinsi gani viwanda hivyo vinaenda kufufuliwa na kuanza uzalishaji kama  vingine kikiwrmo Kiwanda cha Mkwawa Tobacco Leaf Co Ltd .


Mhe. Dkt. Jafo ametoa agizo hilo leo Julai 20, 2024 wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja Mkoani Morogoro ambapo alipata fursa ya kutembelea kiwanda cha Alliance one, Mkwawa Tobacco Leaf Co Ltd, Mazava Fabrics and production East Africa Ltd na kiwanda cha kuchakata mchele cha MW Rice Mills Ltd (KORIE).


Dkt. Jafo amesema kama Wizara ya Viwanda na Biashara wanampango wa kuurudisha Mkoa wa Morogoro kuwa Mkoa wa viwanda kama ilivyokuwa mwazo ili kuwezesha vijana kupata ajira katika viwanda hivyo na kuongeza mapato katika mkoa huo, kuajiri vijana na kuinus uchumi wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.


".. Naomba nimuagize Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara aunde timu ya watu takribani 8 itakayohusisha Mkoa na Msajili wa Hazina (TR) kwenda kuangalia viwanda  ambavyo havifanyi vizuri kuhakikisha vinaiga kiwanda cha Mkwawa Tobacco Leaf Co Ltd kinavyofanya vizuri..." Amesisitiza Dkt. Jafo.


Aidha Dkt . Jafo ameupongeza uongozi wa kiwanda cha Mkwawa Tobacco Leaf Co Ltd kwa uwekezaji mkubwa ambapo  amehimiza kiwe cha mfano wa kuigwa kwa viwanda vingine, huku kiwanda hicho kikizalisha ajira za moja kwa moja 600 na ajira za msimu zaidi ya 3000 ambapo ajira hizo zimepunguza ongezeko la vijana kutokuwa na ajira mtaani.


Aidha, Pia Waziri huyo ameitaka mikoa mingine hapa Nchini kuhakikisha viwanda ambavyo vimekaa muda mrefu bila kufanya vizuri, vinasimamiwa na kuratibiwa ili kuhakikisha vinaanza uzalishaji wa bidhaa ambazo zitaenda kushindana katika soko la kimataifa.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebeca Nsemwa akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemshukuru waziri Jafo kwa kufanya ziara Mkoani humo  na kwamba ziara hiyo itaenda kutatua changamoto  zilizokuwa zikiikabili sekta ya viwanda na biashara.

Sambamba na hilo amemshuruku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka jitihada mbalimbali katika kuhakikisha viwanda Mkoani Morogoro vilivyoacha uzalishaji vinarejea kuzalisha na kuweza kuzalisha ajira kwa vijana.


Naye Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanya biashara Mkoani Morogoro Bw. Mwadhini Mnyanza amesema Mkoa wa Morogoro unajumla ya viwanda 12 ambapo viwanda saba kati ya hivyo havifanyi kazi na viwanda vitano vinafanya kazi ambapo suala hilo Waziri mwenye dhaman amelichukua na kwenda kulifanyia kazi kwa sababu ya umuhimu wake hasa katika suala la ajira kwa vijana na kuongeza mapato Serikalini.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.