• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DKT. MPANGO AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUDHIBITI UHARIBIFU WA MAZINGIRA.

Posted on: November 10th, 2022

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amewataka wakuu wa mikoa, viongozi wa Wilaya na Bodi za Mabonde ya Maji nchini kuhakikisha wanadhibiti uharibifu wa mazingira unaosababishwa na shughuli za kibinaadamu jambo ambalo amesema linachangia kwa kiasi kikubwa upungufu wa kina cha maji katika mito hapa Nchini.

Hapa Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango anasalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa kushoto kwake ni Mhe. Abubakar Kunenge Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango ametoa maagizo hayo Novemba 9, mwaka huu alipotembelea mitambo ya uzalishaji wa Maji Ruvu chini iliyopo mkoa wa Pwani na kisha kupokea taarifa ya hali ya uzalishaji na upatikanaji wa maji katika mikoa ya Dar es na Pwani.

Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akiteta jambo na mwenyeji wake Mhe. Abubakar Kunenge Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa pamoja na viongozi wengine wa mikoa ya Pwani, Dar es salaam na Morogoro.

Aidha, Makamu wa Rais ameitaka Wizara ya Maji kushirikiana na Tamisemi kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya uchimbaji wa visima vya maji na mabwawa ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji hapa nchini.

Sambamba na hayo Makamu wa Rais amekemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya wananchi wasiokuwa waadilifu wanaochoma misitu kwa ajili ya kuandaa mashamba huku akitoa wito kwa wananchi wote kuachana na tabia hizo za uchafuzi wa mazingira kando kando ya vyanzo vya Maji.

Wakuu wa Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro walishiriki kwa pamoja  ziara hiyo ya Makamu wa Rais ambayo ilikuwa na lengo la kudhibiti uharibifu wa Mazingira unaendelea kujitokeza kutokana na shughuli za kibinadam hususan kando kando ya vyanzo vya maji na Mto Ruvu ambao ni tegemeo kubwa la upatikanaji wa Maji Katika Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.