• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Dkt. Mussa akabidhi kompyuta 11 kuboresha huduma za UKIMWI.

Posted on: February 15th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amekabidhi kompyuta 11 pamoja na Vichapishi (printer) kwa Halmashauri 7 za Mkoa huo zikiwa na lengo la kukusanya, kuhifadhi taarifa na kuboresha huduma za UKIMWI katika vituo vya Matunzo na Tiba ya UKIMWI kwenye Halmashauri hizo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi kompyuta hizo leo Februari 15 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Mussa amesema, kompyuta hizo zimenunuliwa na fedha zilizochangwa na wadau mbalimbali wakati wa sherehe za Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambayo Kitaifa zilifanyika Mkoani Morogoro Disemba Mosi, 2023.

Amebainisha kuwa jumla ya fedha zilizokusanywa kwenye maandalizi ya sherehe hizo ni Tsh. 50,000,000/= na baada ya matumizi kwenye sherehe hizo, fedha zilizobaki zimeelekezwa kununua vifaa hivyo ambavyo ni Kompyuta na vichapishi kwa lengo lilelile la kuboresha huduma za masuala ya UKIMWI.  

Katika hatua nyingine Dkt. Mussa amewataka Waratibu wa UKIMWI wa Halmashauri saba zilizokabidhiwa kompyuta hizo kutumia vifaa hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuhamasisha wadau kuendelea kuwa na moyo wa kuchangia.

“...lakini mkazitunze sasa ili zitumike kwa muda mrefu na kuleta manufaa yale yanayotakiwa...” amesema Dkt. Mussa.

Naye Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI, Magonjwa ya Ngono na Homa ya Ini (RASHCo) Mkoa wa Morogoro Dkt. Neema Mtambo amesema kompyuta hizo zitagawanywa katika vituo 11 vya Matunzo na Tiba ya UKIMWI kwenye Halmashauri saba, lengo likiwa ni kuboresha huduma na takwimu za UKIMWI.

Aidha, Dkt. Neema ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujali na kuboresha Sekta Afya huku akiwashukuru wadau waliochangia fedha hizo na kuahidi kuwa atasimamia ili kuhakikisha vifaa hivyo vinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI, Magonjwa ya Ngono na Homa ya Ini kutoka Halmashauri ya Mvomero  Dkt. Grace Emil kwa niaba ya Waratibu wa UKIMWI wa Wilaya amesema vifaa hivyo vitasaidia wananchi kutosafiri umbali mrefu kufuata huduma za UKIMWI na kupata takwimu sahihi na kurahisisha kazi katika Halmashauri hizo.

Halmashauri zilizopata kompyuta na Vichapishi hivyo ni Pamoja na Halmashauri ya Malinyi, Mlimba, Morogoro DC, Ulanga, Mvomero, Gairo na halmashauri ya Kilosa.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RAIS MSTAAFU WA AFRIKA KUSINI AWATAKA WAAFRIKA KUENZI MASHUJAA WAO.

    May 23, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.