• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Dkt. Mussa awaagiza watendaji Kata kuunda Kamati za Usalama.

Posted on: August 16th, 2024


Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali mussa  amewaagiza Watendaji wa Kata kuhakikisha katika Kata zao kunakuwa na Baraza la Usalama la Kata ambalo litaenda kusaidia katika kujadili changamoto na kero mbalimbali zinazowakabili wananchi katika maeneo yao na kuweza kuzitatua kwa wakati.

Dkt. Mussa ametoa agizo hilo wakati akifunga  mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Tarafa na watendaji wa kata wote wa Mkoa wa Morogoro yaliyofanyika katika ukumbi wa mbaraka mwinshehe uliyopo halmashauri ya manispaa ya Morogoro.

Dkt. Mussa amesema Baraza hilo litaundwa na Mtendaji wa Kata, Polisi Kata pia Wenyeviti wa vijiji ambapo amesema baraza hilo  litasaidia kuwakutanisha na kufanya vikao ili kuibua na kutatua changamoto mbalimbali zilizopo katika kata husika.

"..Tulipanga na kuelekeza kwamba katika kila Kata ni lazima kuwepo na kitu kinachoitwa Kamati ya Usalama ya Kata.." Amesema Dkt. Mussa.

Aidha, Dkt. Mussa amewataka watendaji wa Kata na Maafisa Tarafa wote wa Mkoa huo  kufanya kazi kwa umoja na ushirikiano na kila mmoja atekeleze wajibu wake  ili kuweza kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi katika maeneo wanayosimamia kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla kwa sababu wao ni  injini ya maehdeleomhayo.

Aidha, Kiongozi huyo amekemea vikali tabia ya baadhi ya watendaji wa kata kutokaa katika vituo vyao vya kazi ama kukaa mbali na vituo vyao huku akibainisha kuwa hali hiyo inatokana na Maafisa Tarafa kutowasimamia ipasavyo Watendaji hao hali inayosababisha uwepo wa utendaji mbovu wa kazi.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala huyo amekemea baadhi ya viongozi hao wa Serikali  kujihusisha na kupokea rushwa na wengine kuwana tabia za ulevi kitu ambacho kinasababisha kutowajibika katika kazi hivyo amesema hatua kali zitachukuliwa kwa mtendaji yoyote atakaye kwenda kinyume na maadili hayo ya Serikali.

Kwa wao Maafisa Tarafa kupitia Afisa Tarafa wa Mgeta Bw. Fabius Byamungu  wamesema wamejifunza vema masuala ya utawala bora, utunzaji fedha na kuandaa bajeti pamoja na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo  na kwamba amafunzo hayo yataleta chachu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi, hivyo wameishukuru OR- TAMISEMI kwa kuleta mafunzo hayo.

Naye Afisa Mtendaji Kata ya Mafiga Bi. Amina Saidi amesema mafunzo hayo yataenda kuwasaidia katika kutekeleza kazi kulingana na vyeo vyao kama watendaji wa kata, pia yatasaidia katika uwasilishaji wa taarifa ngazi kwa ngazi na kubadili kabisa utendaji wao wa kazi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.