• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Dkt. Samia akubali kujenga hospitali ya rufaa Morogoro.

Posted on: August 6th, 2024



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkat. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Morogoro baada ya ile inayotumika sasa kuonekana inazidiwa katika utoaji wa huduma ya Afya kwa wagonjwa.

Dkt. Samia Suluhu Hassan amebainisha hayo wakati akiongea na wananchi wa Mkoa huo leo Agosti 6, 2024 katika uwanja wa Jamhuri uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Rais Samia amemuagiza waziri mwenye dhamana hiyo Mhe. Ummy Mwalimu na kumtaka atoe shilingi bilioni 5 za kuanzia ili ujenzi huo uanze mara moja hata kama kwa awamu tofauti.

 ".. Nilikuwa na Waziri wa Afya nikampa maelekezo aende akapekue kwenye vifungu vyake angalau apate bilioni 5 za kuanzia na tuanze ujenzi wa hospitali hiyo ya rufaa,

.." amesisitiza Dkt. Samia.

Amesema, fedha hizo shilingi bilioni 5 zianze kujenga majengo ya kutolea huduma ya mama na mtoto na fedha nyingine zitakaletwa baadae zitaendeleze pale walipoishia.

Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo baada ya maombi ya mbunge wa Morogoro mjini Abdul aziz Mohamed Abood kutoa ombi hilo la kupata hospitali ya rufaa ambalo ni ombi la siku nyingi baada ya kuona hospitali inayotumika sasa kuonekana  inazidiwa na wingi wa wagonjwa


Akizungumzia juu ya  Morogoro ya viwanda, Dkt. Samia amesema Serikali ya awqmumya sita imedhamiria kurudisha hadhi ya Morogoro, kuwa Mkoa wa viwanda huku akitaja kufufuliwa kwa kiwanda cha kuchonga vipuli cha mang'ula kilichpo Wilayani Kilombero mkoani humo.

Hata hvyo amesema  lengo la kurejesha mkoa huo kuwa Mkoa wa viwanda ni kutaka kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana Mkoani humo na Taifa kwa ujumla.

Kuhusu utunzaji wa mazingira  Rais Dkt. Samia Suluhu amesema pamoja na umuhimu wa mabonde ya hapa nchini, bonde la Kilombero lina umuhimu zaidi kutokana na bonde hilo kuwa ni moja ya chanzo kikuu cha mradi mkubwa wa kufua umeme katika bwawa la Mwalimu Nyerere.

Hivyo ametoa wito kwa wanamorogoro kulitunza bonde hilo lenye hekta 55 kwa kutoa ushirikiano pale Serikali itakapoanza kutekeleza azma yake ya kulijenga kwa lengo la kuhifadhi maji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na kuzuia mafuriko ambayo kutokea karibu kila mwaka hivyo bonde hilo liweze kuleta raha kwa wananchi badala ya karaha.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amezungumzia Mkoa wa Morogoro kuwa ni Mkoa wa uzalishaji wa mazao ya chakula na kwamba unategemewa na Taifa hususan katika zao la mpunga ambalo linazalishwa kwa wingi kuliko mikoa yote hapa nchini.

Pia amebainisha kuwa Mkoa wa Morogoro una kiwanda cha kuchakata mchele na mmiliki wake ndiye mnunuzi mkubwa wa mchele hapa nchini ambapo ananunua shilingi 900 kwa kila kilo moja.

Kabla ya kufanya mkutano na wananchi wa Morogoro, Dkt. Samia Suluhu Hassan alianza ziara ya leo kwa kuweka jiwe la msingi la kiwanda cha kutengeneza sigara cha Serengeti Cigaratte Company Limited na kisha kuzindua majengo ya maabara jumuishi ya Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine (SUA).


Kesho Agosti 7, 2024 Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anategemea kukamilisha ziara yake ya siku sita (6) Mkoani Morogoro kwa Kuzindua kiwanda cha Sukari cha mkulazi kilichopo Kilosa Mkoani humo.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.