• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Gairo yaitikia mfumo wa Stakabadhi Ghalani.

Posted on: February 9th, 2024

Wajumbe wa mkutano wa Wadau wa masoko ya mazao ya kilimo na mfumo wa stakabadhi ghalani katika Halmashauri ya Wilaya ya Gairo wameupokea kwa mikono miwili uuzaji mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani huku lengo likiwa ni kuinua kipato cha wakulima wenyewe pamoja na Halmashauri hiyo.

Hayo yamebainishwa Februari 8, 2024 na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Rahel Nyangasi wakati wa Mkutano wa Wadau wa masoko ya mazao ya kilimo na mfumo wa stakabadhi ghalani Wilayani Gairo uliolenga kupeana uelewa wa pamoja kuhusu umuhim wa mfumo huo.

Mhe. Nyangasi amesema mfumo huo utaisaidia halmashauri ya Gairo kukusanya mapato mazuri ambapo kabla wanufaika walikuwa ni walanguzi hivyo ameahidi kupitisha azimio hilo kwenye kikao cha baraza la madiwani ili kuupa nguvu mfumo huo, huku akiwataka Madiwani wenzake kufikisha elimu kwa wananchi kuhusu mfumo huo.

“...lakini tunaona kabisa kuwa mfumo huu sisi Halmashauri tutakusanya mapato pamoja na kupunguza matumizi...Mkurugenzi hebu andaeni paper hii kesho bahati nzuri tunalo baraza la Madiwani tuipitishe ili mpango kazi huu uanze kazi mara moja..." amesema Mwenyekiti wa Halmashauri.

Aidha, ameongeza kuwa baraza la Madiwani limeupokea mfumo huo huku akimpongeza Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kubuni vyanzo vya mapato ili kuitoa Halmashauri mahali ilipo sasa.

Awali, akifungua mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame amesema lengo la kikao hicho ni kuwaleta pamoja wataalamu wa masuala ya Stakabadhi ghalani na kutaka Watendaji wa Halmashauri hiyo kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu mfumo huo ili wakulima na Halmashauri hiyo kupata mapato hivyo kukuza uchumi wao na taifa lao.

Ameongeza kuwa, mfumo wa Stakabadhi ghalani utawasaidia wakulima kupata masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi, hivyo amewataka wajumbe wa mkutano huo kuhamasisha wananchi juu ya umuhim wa mfumo huo katika shughuli zao za kilimo.

Kwa upande wake Meneja wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala Bw. David Sukali amesema Mkoa wa Morogoro kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghalani umewaingizia wakulima zaidi ya shilingi 12 bilioni kwa mazao ya mbaazi, ufuta na kakao huku akibainisha kuwa mfumo utawasaidia wakulima kuwa na sauti moja ya kuamua nani wamuuzie na kwa bei gani, lakini pia kuwa na uhakika wa soko kwa mazao yao.

Nao baadhi ya wakulima Wilayani humo akiwemo Mhe. Butindi Masatu ambaye ni Diwani Kata ya Kibedya ameipongeza Serikali kwa kuja na mfumo huo ambao ni suluhisho kwa wakulima na kuwaomba wadau kuyapa kipaumbele mazao yanayolimwa kwa wingi katika Wilaya hiyo yakiwemo mazao ya Ufuta, mbaazi na maharage.

Wajumbe wa kikao hicho waliazimia kuyaingiza mazao manne ya Ufuta, Korosho, Mbaazi na Maharage kwenye mfumo wa Stakabadhi ghalani ili wakulima waanze kufaidika kupitia mazao hayo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.