• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Hakuna mkandarasi atakayelipwa mpaka barabara zitakapo tengenezwa vizuri kwa kiwango kinachokubalika kitaalam..Fatma Mwassa RC Morogoro

Posted on: October 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa ameagiza Wakala wa Baraba za Mijini na Vijini (TARURA) kutomlipa mkandarasi anayejenga barabara ya Kijiji cha Lulongwe, Kata ya Matuli Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kutokana na barabara hiyo kutojengwa kwa kiwango kinachostahili.

Fatma Mwassa ametoa agizo hilo Oktoba 21, mwaka huu wakati wa ziara fupi aliyoifanya katika kata hiyo ya Matuli kwa lengo la kukagua na kujionea ujenzi wa barabara hiyo baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi juu ya ujenzi wa barabara hiyo usioridhisha.

Amesema, hajaridhishwa na ujenzi wa barabara hiyo kutokana na kuwepo wa dosari nyingi katika ujenzi huo, hivyo TARURA na wataalamu wote wa barabara Mkoani humo wakae kikao cha pamoja kujadili dosari hizo na mkandarasi asilipwe hadi pale atakaporekebisha dosari hizo.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu  Mhandisi Ezron Kilamhama kikagua karavati ltakalo tumika katika ujenzi wa daraja katika kijiji cha Lulongwe.

“...kwa hiyo zote hizo dosari zitarekebishwa kwanza ndipo mkandarasi awezekuchukua pesa yake, hakuna mkandarasi hata mmoja atakayelipwa bila kuwa hizi barabara zimetengenezwa vizuri kwa kiwango kinachokubalika kitaalam...” amesema Fatma Mwassa.

Sambamba na hilo Fatma Mwassa ametoa miezi miwili kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kuhakikisha Zahanati ya Lulongwe inapatiwa vifaa tiba kwa kuwa ujenzi wa zahanati hiyo umekamilika huku akimtaka Mkuu wa Wilaya hiyo kusimamia agizo hilo.

Kwa upande wao wakazi wa Kijiji cha Lulongwe akiwemo Bw. Rosta Salumu wameishukuru Serikali kutatua changamoto za wananchi kwa wakati wakiwemo wa kijiji hicho, hata hivyo wamemueleza Mkuu wa Mkoa tatizo la kijiji chao la kutoitisha mikutano ya hadhara kama inavyotakiwa, hivyo hawajawahi pia kusomewa taarifa ya mapato na matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali.

Nae Diwani wa Kata ya Matuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mhe. Lucas Lemomo amekiri kutokuwepo kwa mikutano ya hadhara katika Kijiji hicho na kuhaidi kuifanyia kazi changamoto hiyo.

Mkuu wa Mkoa Fatma Mwassa alifanya ziara fupi katika Halmashauri hiyo baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi juu ya  utekelezaji wa miradi ya maendeleo usioridhisha hususan katika kijiji cha Lulongwe ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara ya kijiji hicho na ujenzi wa Zahanati ambapo pia alikutana wananchi na kujibu baadhi ya kero zinazowakabili.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.