• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Halmashauri ya Ifakara kujenga kituo cha Afya kwa Mapato yake ya ndani.

Posted on: July 23rd, 2022


Halmashauri ya Mji wa Ifakara Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro imetenga zaidi ya shilingi Milioni 400 kutoka Katika Mapato yake ya ndani kujenga kituo Cha Afya Cha Kata ya Mbasa kwa lengo la kunusuru maisha ya mama na mtoto pamoja na kutoa huduma nyingine za Afya kwa wananchi zaidi ya 6,000 wa kata hiyo.

Hayo yamebainishwa hivi karibuni wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela, alipofanya ziara Wilayani humo kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kukagua ujenzi wa kituo cha Afya kinachojengwa katika Kata ya Mbasa.

Kituo hicho ambacho hadi sasa kimefikia asilimia 94, ujenzi wake umetanguliwa na jengo la Mama na Mtoto kwa lengo la kunusuru maisha ya kundi hilo la mama na mtoto kwa kutumia fedha zake zinazotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo ya Mji wa Ifakara.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akiongea wakati akikagua jengo hilo la mama na mtoto Mara baada ya kukamilisha ziara yake Katika Halmashauri ya Mlimba, amewahakikishia wananchi wa Kata ya Mbasa kuwa Serikali italeta madawa, vifaa tiba na wahudumu ili wananchi wa kata hiyo na kata jirani waweze kupata huduma waliyoitarajia.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ifakara na Wataalamu wake wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Hanji Godi godi kwa kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan la kuzitaka Halmashauri zote hapa nchini kila moja kujenga Kituo kimoja cha Afya kupitia mapato yake ya ndani.

“Huduma hii ya Afya ni miongoni mwa maeneo yanayopewa kipaumbele na Serikali hii ya awamu ya sita, niwahakikishie wananchi wa Ifakara kwamba Serikali italeta madaktari wa kutosha ili kutoa huduma katika kituo hiki cha Afya”amesema Martine Shigela

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Hanji Godigodi ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha wazo la kila Halmashauri kujenga jengo kuanzia msingi hadi kulikamilisha ili mapato ya ndani yaweze kuonekana kwa urahisi kwa wananchi.

“ujenzi umeshakamilika kwa asilimia 90, tunategemea hivi karibuni baadhi ya majengo yataanza kutumika” amesema Godigodi.

Naye Diwani wa Kata hiyo, Mhe. Khadija Rashid Kilama ameishukuru Serikali kwa kufanikishia ujenzi wa kituo cha Afya cha Mbasa ambapo hapo awali katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara kulikuwa na vituo vya Afya viwili kikiwemo cha Serikali kimoja na cha binafsi kimoja hali yoilipelekea wananchi wa hali ya chini kushindwa kupata huduma ya Afya kutokana na galama kubwa.

Diwani wa Kata ya Mbasa, Mhe. Khadija Kilama.


Sambamba na hayo amesema kujengwa kwa kituo hicho cha Afya kitakipunguzia mzigo kituo cha Afya cha Kibaoni na hivyo kumfanya Mwananchi wa chini kupata huduma za matibabu kwa gharama nafuu na haraka zaidi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.