• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi yatakiwa kuwashirikisha wananchi.

Posted on: August 6th, 2021

Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro wametakiwa kujijengea tabia ya kuwashirikisha wananchi wa eneo husika fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayofanyika katika maeneo yao ili kuwa na uelewa na miradi hiyo, kuanza na kukamilika kwaake.

Agizo hilo limetplewa Agosti 5 mwaka huu na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Lt. Josephine Paul Mwambashi mara baada ya kuweka jiwe la Msingi  katika mradi wa Zahanati  ya Minepa inayojengwa baada ya Serikali kutoa pesa na wananchi kuchangia nguvu zao.

Aidha, Lt. Mwambashi amesema, wananchi wanastahili kufahamishwa kila hatua ya maendeleo ya miradi inayofanyika katika maeneo yao kwa sababu wao ndio walengwa katika ujenzi wa miradi hiyo.

Amesema fedha za miradi hiyo inayotolewa kwa ajili ya miradi kama hiyo ziwe zinakwenda moja kwa moja kwenye akauti ya kijiji husika badala ya kwenda Halmashauri ya Wilaya kwa kuwa fedha hizo zinakuwa za wananchi hao hivyo waachiwe kufanya kazi za utekelezaji wa miradi hiyo mwenyewe.

‘’Tumepita katika miradi mingi ambayo wananchi wakipewa ile pesa watendaji katika vijiji wanasimamia vizuri kwa sababu wanajua umuhimu wa vituo vya Afya na zahanati kwa wananchi, nasisitiza kwamba pesa zikija msiig’ang’anie Halmashauri waachieni wananchi wajisimamie’’ amesema Lt. Mwambashi.

Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi la zahanati hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ulanga  Ngolo Malenya amempongeza kiongozi huyo wa mbio  za Mwenge kwa kuweka jiwe la msingi na kumuahidi kusimamia maelekezo yote aliyoyatoa.

Ngolo Malenya amesema kwa kipindi kirefu wananchi wa Kijiji cha Minepa wamekuwa wakipata changamoto ya kupata huduma ya Afya huku wakilazimika kwenda umbali mrefu kwa ajili ya kupata huduma hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji hicho akiwemo Bi. Joyce Samwel wameonekana kufurahishwa na ujenzi wa zahanati hiyo na kubainisha kuwa hiyo itakuwa suluhu ya changamoto  ambazo wamekuwa wakikumbana nayo hususan kwa mama wajawazito.

Naye, James Mussa mkazi wa kijiji hicho, ameishukuru Serikali kwa kuleta fedha za zahanati hiyo ili kupata huduma ya Afya karibu kwani amesema wananchi hususan akinamama wajawazito wameteseka kwa muda mrefu kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya Afya hata wakati mwingine kusababisha akinamama hao kujifungua  njiani.

‘’Mama wajawazito wanasumbuka sana wanapokaribia kujifungua kwa sababu hospitali ya kivukoni ipo mbali sana kiasi kwamba mama wajawazito hujifungulia njia kutokana na umbali, naamini kituo hiki sasa kitatusaidia ’’ amesema Mussa.

Mwenge wa Uhuru 2021 umekamilisha kupitia jumla ya miradi sita ya maendeleo Wilayani Ulanga Mkoani  humo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bil. 8.5 bila kuwepo kikwazo chochote.

Mwenge wa uhuru wa mwaka 2021 wenye Kauli Mbiu: “TEHAMA ni Msigi wa Taifa Endelevu Itumike kwa Usahihi na Uwajibikaji” uanendelea kukimbizwa Mkoani Morogoro ikiwa ni siku ya tatu tangu kuingia Mkoani humo.

 

MWISHO 

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.