• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Halmashauri zote nchini zatakiwa kuandaa utaratibu wa uuzaji viwanja.

Posted on: July 14th, 2021

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula  amezitaka Halmashauri zote nchini kuandaa utaratibu mahususi  wa uuzaji na ununuaji wa viwanja  utakaohusisha viongozi wa Halmashauri husika wakiwemo watendaji ngazi ya vijiji/mitaa  ili kupunguza migogoro ya Ardhi inayoendelea kujitokeza.

Naibu Waziri ametoa kauli hiyo Julai 13 mwaka huu wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku ya pili Wilayani Morogoro kwa ajili ya kusikiliza na kutatua migogoro ya Ardhi inayowakabili wananchi wa Manispaa hiyo.

Dkt. Mabula amesema endapo Viongozi wa Halmashauri wakiwemo Watendaji wake wakawa sehemu ya uuzwaji wa kila kiwanja ni wazi kuwa migogoro hiyo ya Ardhi itapungua au kuisha kabisa kwa kuwa kutakuwa hakuna udanganyifu baina ya pande mbili yaani mnunuaji na muuzaji baina ya pande hizo mbili.



“…Halmashauri andaeni utaratibu wa kuwa na fomu, kama kuna mtu ana eneo lake ndani ya Mji anataka kuliuza ni lazima pia nyie muwe sehemu ya uuzwaji wa eneo hilo ili kutambua hilo eneo ni mmiliki halali, mkiweka utaratibu huo hakuna mtu atauza eneo bila kufuata utaratibu. ….’’amesema Dkt. Mabula.

 Katika hatua nyingine Dkt. Angelina Mabula amezitaka Halmashauri zote nchini kupitia upya kesi zote zinazohusu migogoro ya Ardhi ambayo inahusisha Watendaji wa Serikali na wananchi kuhakikiwa ili kupata ukweli halisi na kutoa haki kwa yule anayestahili.

RAS Morogoro Bi. Mariam Mtunguja akisikiliza kero za wananchi zinazotolewa mbele ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula.

“…Niombe watumishi wa Halmshauri zote nchini, popote nitakapokuta kuna kesi ya mgogoro wa Ardhi baina ya kiongozi na mtu wa kawaida, na mtu wa kawaida umemkuta pale  maana yake hiyo hati nitataka ibatilishwe…” amesema Dkt. Mabula. 

Akizungumzia suala la urasimishaji wa Ardhi, Dkt. Mabula amempongeza Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuruhusu wananchi kurasimishiwa maeneo yao ambayo walijenga na kufanya makazi yao kwa muda mrefu huku akibainisha kuwa maeneno hayo hawatapewa wananchi ambao wamejenga hivi karibuni.

RC Morogoro Martine Shigela (kulia) na DC  Morogoro Albert Msando wakisikiliza kero za wananchi wa Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na wananchi hao Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela, ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutenga bajeti kwa ajili ya kupima maeneo yenye migogoro yakiwemo ya Kihonda na Mkundi ili katika maeneo hayo kila mwananchi atambue mpaka wake.

Aidha, Shigela amebainisha kuwa mara baada ya Manispaa kupima maeneo hayo wananchi watafikishiwa huduma zote muhim kiwemo huduma ya maji, ujenzi wa vituo vya Afya, soko, stendi ya mabasi na miundombinu ya barabara lengo ni kuwasadia wananchi hao kufanya shughuli zao za maendeleo bila kuwa na changamoto zozote.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando, amempongeza Dkt. Angelina Mabula Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kutatua kero ndani ya Wilaya hiyo na kumuahidi kutekeleza maagizo yote ambayo ameyatoa.

Naye, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Morogoro Frank Mizikuntwe amewataka wanachi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuacha tabia ya kujenga maeneo ya milimani ili kutunza mazingira, kutunza vyanzo vya maji na taka ambazo zingezalishwa na wakazi wake na kusababisha  bwawa la Mindu kupungua kina chake.


Wananchi wa Manispaa ya Morogoro wakiwa wamejipanga kuwasilisha kero zao kwa Mhe. Naibu Waziri.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi walioshiriki Mkutano huo akiwemo Valentine Cosmas na Maria Michael wamesema migogoro mingi iliyopo katika halmashauri ya Manispaa hiyo inatokana na viwanja kuuzwa zaidi ya mara mbili (double allocation) ambapo husababishwa na baadhi ya viongozi wa Serikali wasio waaminifu.

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.