• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

HEWA UKAA RAFIKI KWA MAZINGIRA.

Posted on: February 24th, 2023


Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro

Wataalam wa mazingira Mkoani Morogoro wameshauri watu binafsi, taasisi, mashirika na kampuni binafsi nchini kujihusisha na biashara ya hewa ukaa kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambayo yanaleta athari kwa binadamu.

Ushauri huo umetolewa Februari 23 mwaka huu na wajumbe mbalimbali walioshiriki kikao cha elimu juu ya biashara ya hewa ukaa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Akifafanua juu ya dhana ya mabadiliko ya tabianchi, Mkurugenzi wa kituo cha Kitaifa cha kufuatilia Kaboni Prof. Eliakimu Zahabu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) amesema kwa sasa Tanzania inakabiliwa na athari za mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ongezeko la joto, ukame, mafuriko, n.k. huku akibainisha kuwa hayo yote yanatokana na uharibifu wa mazingira ikiwemo ukataji wa miti ovyo.

Aidha, Prof. Zahabu ambaye  alikuwa ndiye mtoa mada mkuu wa kikao hicho amesema biashara ya hewa ukaa ni mfumo katika soko la dunia ambao unasadia kupunguza gesi joto angani ambayo inatokana na shughuli za viwanda na uchomaji wa moto na ukataji wa miti na uharibifu wa misitu iliyopo.

Mtoa mada prof. Eliakimu Zahabu akielezea kuhusu umuhimu wa biashara ya kaboni.

“...biashara hiyo inahusisha upandaji na utunzaji wa miti na kuweka mifumo inayodhibiti uzalishaji wa hewa hiyo katika shughuli mbalimbali ikiwemo za kilimo, nishati, viwanda, na miundombinu...” amesema Prof Zahabu.

Nae, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa baada ya mawasilisho na majadiliano ya mada mbalimbali zinazohusu biashara hiyo akaeleza maazimio ya kikao hicho, ikiwa ni pamoja na moja kati ya maazimio hayo ni kuundwa kwa kamati ya mazingira ya Mkoa ambayo itajishughulisha na utunzaji, uhifadhi na udhibiti wa uharibifu wa mazingira katika Mkoa huo.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kamati hiyo itakuwa chini ya mwenyekiti Mhe. Dkt. Julius Ningu ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ulanga na itahusika na masuala ya biashara ya kaboni, uhifadhi na utunzaji wa wazingira kwa ujumla.

Mhe. Dkt. Julius Ningu Mkuu wa Wilaya ya Ulanga ameteuliwa na Mkuu wa Mkoa kuwa mwenyekiti wa kamati ya Mazingira ya Mkoa..

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame amesema elimu waliyoipata kuhusu biashara ya kaboni ni fursa muhimu kwa serikali, watu binafsi, taasisi na wananchi kunufaika na mapato ya biashara hiyo pamoja na utunzaji wa mazingira na kupendekeza kuwa ili kufanikisha hilo, elimu inatakiwa itolewa kwa wananchi na viongozi ili kuwa na uelewa wa pamoja

Baada ya kikao hicho, wajumbe, waliazimia kuwa Halmashauri zote mkoani humo ziainishe misitu ya vijiji inayoweza kuingizwa kwenye biashara ya kaboni na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu biashara hiyo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.