• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

IFIKAPO DISEMBA MWAKA HUU VIJIJI VYOTE MOROGORO KUPATIWA UMEME.

Posted on: October 28th, 2024



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu ( Kazi Maalum) Captain mstaafu Mhe. George Mkuchika amesema Wakala wa Nishati ya Umeme Vijijini (REA) wamefanikiwa kupeleka huduma ya nishati ya Umeme katika Vijiji 652 kati ya vijiji 666 vya Mkoa wa Morogoro na kukamilisha huduma hiyo kwa vijiji vilivyobaki ifikapo Disemba Mwaka huu.

Mhe. kuchika amebainisha hayo Oktoba 28, 2024 wakati akiwasha umeme katika kijiji cha Magenge kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Gairo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua, kuzindua na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya sita katika Mkoa huo.

Aidha, Waziri Mkuchika amesema Serikali ya CCM inajukumu la kuhakikisha kero ya ukosefu wa umeme kuondoka ambapo Wilayani humo usambazaji wa nishati ya umeme umebakia vijiji 3 pekee vilivyobaki havijapata umeme hivyo ifikapo Disemba, Mwaka huu vijiji vyote vya Mkoa huo vitakuwa vimepata umeme.

".. Na hili la umeme nataka niwaambie wanagairo msiwe na wasiwasi ilani ya uchaguzi imesema hadi kufika Disemba Mwaka  huu vijiji vyote viwe vimepata umeme..." amesema Mhe. George Mkuchika

Waziri huyo amesema Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi ambapo katika kata ya Iyogwe imetoa shilingi Mil. 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya, Mil. 518 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari, Mil. 500 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maji na Mil. 500 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na daraja ili kusogeza huduma muhimu kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema katika Mkoa huo wenye jumla ya vijiji 666 ambapo vijiji 649 vimefikiwa kupata huduma ya umeme na vijiji 17 vipo katika hatua za ukamilishwaji ambapo matarajio ya Mkoa huo ni vijiji vyote 666 kupata huduma ya umeme ili kuanza kazi ya kusambaza umeme kwenye vitongoji.

Naye Meneja wa TANECSO wa Wilaya ya Gairo Mhandisi Gilles Daniel akisoma taarifa ya Wilaya hiyo amesema kijiji cha Magenge ni moja kati ya vijiji nane katika Kata ya Madege ambapo mradi huo unagharamu ya zaidi ya Bilioni 5.4 hivyo ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha hizo kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji vya Wilaya ya Gairo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.