• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

JUMUIYA YA WAISLAMU WA AHMADIYYA MOROGORO YATOA MSAADA WA VYAKULA KWA ZAIDI YA KAYA 110 ZENYE UHITAJI.

Posted on: May 11th, 2022

JUMUIYA ya Kiislamu ya Ahmadiyya Morogoro imetoa msaada wa zaidi ya Kaya 110 zenye uhitaji zilizopo Kata ya Kihonda Maghorofani Manispaa ya Morogoro ikiwa ni chakula kwa ajili ya Mkono wa Eid Fitri ambapo utaratibu huo umekuwa ukifanyika kabla ya Sikukuu.



Hafla hiyo fupi ya ugawaji wa vyakula imefanyika Mei 09/2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ahmadya Kihonda Maghorofani.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo la ugawaji wa vyakula, DC Msando, ameomba mashirika na Taasisi zingine yakiwemo madhehebu ya dini kuelekeza misaada mbalimbali kwa wananchi wenye uhitaji maalumu ili kutengeneza furaha na kudumisha umoja baina yao na wenye uhitaji.





DC Msando,ambaye ndiye mgeni rasmi wa hafla hiyo fupi ya ugawaji wa chakula kwa wenye mahitaji akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Martine Shigela, amesema Ahmadiyya wamefanya jambo la Uchamungu ambalo linatakiwa liigwe na Taasisi nyengine.




Naye Mkuu wa Chuo cha Jumuiya ya Ahmadiyya Morogoro, Sheikh Abid Mahmood Bhatti, amesema kuwa msaada huo umetolewa kuunga mkono wito wa Serikali inayohimiza mashirika, taasisi, na watu binafsi kutoa misaada kwa jamii yenye uhitaji.





Bhatti, amesema licha ya kuunga mkono Serikali lakini pia kuweza kutoa zakatul Fitri kwa jamii ili kuweza kujumuika na jamii katika kusherehekea Sikukuu ya Eid Fitr ambayo tayari imeshapita japo wamekuwa wakifanya kabla ya Sikukuu.

"Jumuiya ya Ahmadiyya ni moja ya sehemu inayojihusisha na utoaji wa misaada mbalimbali ikiwemo ya kiafya,kielimu na kijamii kwa kuwafikia watu wenye uhitaji, hivyo kutoa kwetu chakula kwa watu wenye uhitaji kwanza tumetekeleza misingi ya dini , kwani sisi tumekuwa tukifanya hivi kila ifikapo Siku ya Eid basi tumekuwa tukijumuika na ndugu zetu kuhakikisha kwamba tunakuwa nao pamoja katika kusheherekea sikukuu hii." Amesema Bhatti.



Miongoni wa vyakula hivyo vilivyo gharimu takribani Shilingi Milioni 2 na laki 5, ni pamoja na Mchele mfuko wenye Kilo 5 na Unga wa Sembe Mfuko wa Kilo 10 kwa kila Kaya.




MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.