• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KAIMU RAS MOROGORO ASISITIZA MATUMIZI SAHIHI TSH. 4.7BIL. MRADI WA AFYA YANGU.

Posted on: December 11th, 2024



Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Rozalia Rwegasira amewataka wenyeviti wa Halmashauri za  Mkoa huo pamoja na Wakurugenzi watendaji wa halmashauri, kuhakikisha wanasimamia kikamilifu fedha shilingi Bil. 4.7 zilizotolewa na Shirika la USAID kupitia mradi wa US AID Afya yangu unaolenga kutokomeza maambukizi ya  Virusi vya Ukimwi (VVU) na Kifua kikuu.

Dkt. Rozalia ametoa agizo hilo Disemba 10, 2024 wakati akishuhudia hafla fupi ya utiaji saini wa mikataba baina ya Mtekelezaji Mkuu wa mradi wa USAID Afya Yangu (My Health) Deloitte Consulting Limited na Halmashauri za Mkoa wa Morogoro, hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Dkt. Rozalia ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Idara ya Uchumi na Uzalishaji Mali akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt. Mussa Ali Mussa amesema, lengo la Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kutokomeza magonjwa ya VVU na Kifua Kikuu na akabainisha lengo la mradi huo kuwa ni kuimarisha utoaji wa huduma za afya ndani ya jamii kwa kuboresha uhusiano baina ya jamii na vituo vya Afya, hivyo amesisitiza matumizi sahihi ya fedha hizo.

".. Naomba kila mmoja wetu akatimize wajibu wake na suala la msingi niwasisitize matumizi sahihi ya hizi fedha kulingana na malengo yaliyotarajiwa.." Amesisitiza Dkt. Rozalia.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa fedha na Utawala wa shirika la Diloitte Consulting Limited linalosimamia mradi wa USAID Afya Yangu Bw. Erick Mwelulila amesema, mradi huo unatekelezwa katika mikoa sita ya Iringa, Morogoro, Lindi, Mtwara, Njombe na Ruvuma ambapo Mkoa wa Morogoro umepewa jumla ya shilingi Bilioni 4.7 zitakazotumika katika Halmashauri zote tisa kupitia mradi huo.

Naye Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga ameishukuru USAID kwa kuja na mradi huo na kuiamini Serikali, hivyo amewataka viongozi wanaosimamia fedha hizo kuhakikisha wanazisimamia vizuri ili kuweza kujenga uaminifu huku akiahidi kwenda kutekeleza majukumu ipasavyo kama walivyoaminiwa na Shirika hilo.

Mradi wa USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini unalenga kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya zinazomlenga moja kwa moja mtumiaji, kuboresha uwezo wa mtu binafsi kuwa na tabia njema na kusaidia mazingira wezeshi ya utoaji wa huduma bora za afya.



MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.