• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Morogoro kuimarisha ushirikiano na Zanzibar katika nyanja ya kilimo

Posted on: October 16th, 2025


Mkoa wa Morogoro na Zanzibar imeendelea kukuza ushirikiano kwenye masuala ya kilimo hususan katika kilimo cha Karafuu na Mpunga ili kuongeza utaalamu kwa pande hizo mbili na hivyo kuongeza uzalishaji wa mazao hayo na kupata masoko.

Hayo yalibainishwa Septemba 15, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati akifunga ziara ya mafunzo ya Maafisa ughani mafunzo kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyofanyika katika ukumbi wa TARI wa kuoneshea teknolojia ya Kilimo uliopo Nanenane Mkoani Morogoro.

Mkoa umepokea maafisa 33 ambao wametembelea mashamba mbalimbali ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) kwa lengo la kujifunza mbinu bora za kilimo cha mazao mbalimbali.



Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema ushirikiano wa pande hizo mbili ni muhimu kwani Morogoro inahitaji masoko ya mazao hususan Mpunga na Karafuu na Zanzibar inahitaji bidhaa hususan zao la mchele hivo ni vyema pande hizo mbili zikaongeza ushirikiano wa sekta ya kilimo ili kuhakikisha upatikanaji wa mchele Zanzibar unaongezeka.


“Ninyi leo tunawakaribisha mjionee kama mpo sehemu ambayo katika mahusiano haya, mnatuhitaji na sisi tunawahitaji. Ninyi mna masoko, sisi tuna uzalishaji,”

amesema Mheshimiwa Adam Kighoma Malima.


Aidha amesema, Mkoa wa Morogoro kwa sasa ndio unaoongoza nchini kwa uzalishaji wa mchele, ambapo huzalisha tani 600,000 kwa mwaka wakati Zanzibar inazalisha tani 50,000 pekee huku uhitaji wake ukiwa tani 120,000 na kwamba ushirikiano huo utasaidia kuongeza uzalishaji wa mpunga visiwani humo kupitia mafunzo na mbinu bora zinazotumika katika Mkoa wa Morogoro.


Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amewaalika Maafisa hao ughani 33 kurudi Morogoro kufanya ziara kama hiyo hususan katika maeneo yaliyopo Mkoani humo yanayozalisha Mpunga kwa wingi ikiwemo Wilaya ya Kilombero na Malinyi maeneo ambayo hawakufika kwa sababu ya  kuwa na siku chache za Ziara yao lengo ni kujifunza zaidi kwa vitendo.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uhaulishaji wa Teknolojia na Mahusiano (TARI), Dkt. Sophia Kashenge amesema, lengo la ziara hiyo ni kubadilishana uzoefu katika uzalishaji wa mazao mbalimbali na kubainisha kuwa TARI imeendelea kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Zanzibar (ZARILI) katika kuboresha mbinu za kilimo cha mazao ya chakula na biashara ili kuongeza tija na uzalishaji visiwani humo.


Dkt. Kashenge ameongeza kuwa ushirikiano huo hautaishia kwenye maneno pekee, bali utaendelezwa hadi kufikia hatua ya kuingia makubaliano ya maandishi, yenye malengo ya pamoja ya kuongeza uzalishaji kupitia tafiti mbalimbali za kilimo.


Naye Afisa Ughani Mkuu kutoka Zanzibar, Dkt. Salum Rehani, ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Morogoro kwa kuwapokea na kuwapatia mafunzo hayo muhimu. Amesema wamejifunza mbinu mpya ya kitalu mkeka, ambayo haijaanza kutumika Zanzibar, na kwamba ujuzi huo utasaidia kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga visiwani Zanzibar.


Kwa upande wake, Afisa Uzalishaji kutoka Idara ya Umwagiliaji Maji, Bi. Rukia Mohamed, amesema wamejifunza umuhimu wa kutumia mbegu bora kulingana na misimu ya kilimo (vuli na masika), jambo ambalo awali halikuzingatiwa na kubainisha kwamba watayafikisha mafunzo hayo kwa wakulima wa Zanzibar ili waweze kutumia aina sahihi za mbegu na kwa msimu husika.


Katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mheshimiwa Adam Kighoma Malima alipata pia fursa ya kuzindua kisima cha maji cha kituo cha Uhaulishaji wa Teknolojia ya masuala ya kilimo - TARI, kilichochimbwa kwa ushirikiano na Serikali ya Mkoa ambacho kitarahisisha upatikanaji wa maji katika kituo hicho kilichopo Nanenane Manispaa ya Morogoro.



Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kuimarisha ushirikiano na Zanzibar katika nyanja ya kilimo

    October 16, 2025
  • Morogoro kuanzisha jarida la programu ya PJT–MMMAM

    September 30, 2025
  • Viongozi wa Serikali Mkoani Morogoro watakiwa kulinda UHAI wa Bonde la Kilombero.

    September 26, 2025
  • Gairo kuanza kuhamasisha kilimo biashara.

    September 25, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.