• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kamati ya Kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara, kilimo na Mifugo yaagiza kuvunjwa Mkataba wa Mradi wa Skimu Mgongola.

Posted on: February 16th, 2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo wameeleza kutoridhishwa na utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa skimu ya umwagiliaji ya Mgongola Wilayani Mvomero hivyo kuagiza kuuvunja baada ya mkandarasi wake kushindwa kukamilisha kwa wakati.

Kamati hiyo imetoa maagizo hayo Februari 16, Mwaka huu kupitia Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Mariam Mzuzuli (MB) kwa niaba ya Mwenyekiti na wajumbe wake walipotembelea skimu hiyo ikiwa ni siku ya pili ya ziara yao Mkoani Morogoro.

Makamu Mwenyekiti huyo wa kamati amesema mradi huo wenye thamani ya Shilingi bilioni 5.6, unahusisha hekta 620 zinazopata maji kutoka Mto Mkindo katika Kijiji cha Bungoma umekuwa ukisuasua kutokana na mkandarasi M/S BARD EAST AFRICA ENTERPRISES LIMITED aliyekabidhiwa mradi huo mwaka 2022.

 "Mkataba huu unasimamiwa na sheria na mkandarasi ameshindwa kutekeleza wajibu wake, Tunapendekeza hatua zichukuliwe mara moja," alisema Mzuzule.

Aidha, Makamu Mwenyekiti huyo amependekeza kuvunjwa kwa mkataba huo na hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi ya mkandarasi, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha anawajibika kwa hasara yoyote iliyojitokeza kwa wananchi na serikali.


Kwa upande wake, Mhandisi Ezra Chiwesela ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati hiyo (MB) amesema ucheleweshaji wa mradi huo umeibua changamoto kwa wakulima wa eneo hilo huku akiwataka watendaji wa serikali kushirikiana na viongozi wao wa ngazi za juu ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango.


Kwa sababu hiyo, Menejimeti hiyo imeazimia kuvunja mkataba wa mkandarasi huyo baada ya kujiridhisha kutokuwa na nia njema na utekelezaji wamradi huo na kuwaathiri wananchi kiuchumi na kushindwa kufikia malengo yao.


Awali akimkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema mradi huo una manufaa kwa Taifa zima ukilenga kuwa mradi wa mfano kwa Mikoa mingine hivyo Serikali haitafumbia macho jambo hilo na kuiomba Kamati hiyo kulighugulikia suala hilo.


Naye, Mhandisi wa umwagiliaji wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Mattanga Juma akitoa taarifa ya mradi huo amesema tayari ameshautolea taarifa ngazi za juu kuhusu kusuasua kwa mradi ikiwemo menejimenti ya Tume ya Taifa ya umwagiliaji kuiitisha vikao mara tatu kujadiliana na mkandarasi ili kunusuru mradi huo.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.