• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kamati ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yajipanga

Posted on: July 19th, 2022

Kamati ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yajipanga

Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya wakulima - Nanenane Kanda ya Mashariki inayoundwa na Mikoa minne ya Dar es salaa, Pwani, Tanga na wenyeji Morogoro imeendelea na vikao vyake vya maandalizi ya Maonesho ya mwaka huu 2022 Mkoani Morogoro, lengo likiwa ni kufikia ufanisi mkubwa wa maonesho hayo kuliko miaka ya nyuma.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima wakati akiongoza kikao cha wataalamu na viongozi wengine kwa ajili ya maandalizi ya sherehe hizo kilichofanyika Mkoani Morogoro katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ukumbi wa Jeshi la Kujenga Taifa - JKT uliopo Nanenane.


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima akitoa wito kwa  wananchi wa Kanda ya Mashariki mara baada ya Kikao cha Kamati ya maandalizi ya Kanda hiyo, kujitokeza na kushiriki Maonesho ya Nanenane ili kupata elimu bora ya ufugaji, uvuvi na ukulima.


Mkuu huyo wa Mkoa amesema kupitia ushindani wa ndani uliopo baina ya Mikoa ya Kanda hiyo ya Mashariki itapelekea kujiandaa vema na kuhakikisha Maonesho hayo sio yatafana tu bali pia kushinda Kanda nyingine za Maonesho hayo na kushika nafasi ya kwanza Kitaifa.

“Sasa ndio maana tupo kwenye vikao vya Kamati ili kuhakikisha tunapata utekelezaji Madhubuti kuweza kufikia malengo tuliojiwekea na hatimaye kushika namba 1 kitaifa” amesema Malima.


Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa Adam Malima ameendelea kutoa wito kwa wananchi wa Mkoa Morogoro, Pwani, Dar es Salaam na Tanga pamoja na Mikoa jirani kujitokeza kushiriki Maonesho hayo na kuchangamkia fursa za kupata elimu na teknolijia mpya za Kilimo, Ufugaji na Uvuvi huku akiwataka wale wanaoleta bidhaa za maonesho kuleta bidhaa zenye ubora ili kunogesha maonesho hayo wakiwemo wanyama kama vile simba na wanyama wengine.



Baadhi ya vipando vilivyopo katika uwanja wa Maonesho wa MWL. J.K. Nyerere kama sehemu ya Maandalizi ya Maonesho hayo kwa mwaka huu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albart Msando ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya hiyo na Tanzania kwa ujumla kujitokeza na kufika katika Banda la Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kujionea jinsi wakulima wa mijini watakavyoweza kutumia ardhi kidogo ya kulima kwa tija.


Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albart Msando akipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya kilimo wa Hamashauri ya Manispaa ya Morogoro Michael Waluse ya namna ya kutumia Ardhi kidogo kwa kilimo chenye tija.





Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Kilimo wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Bw. Michael Waluse ameweka wazi kuwa kuna umuhimu wa wakulima kuweza kutumia teknolijia ya umwagiliaji kwa njia ya matone ya maji ili kuweza kutunza na kuhifadhi maji kwa ajili ya matumizi mengine ya kibinadamu lakini pia kuokoa gharama kubwa kwa mkulima.


Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Maandalizi Kanda ya Mashariki ya Maonesho Nanenane kutoka Mikoa minne ya Morogoro, Tanga, Pwani na Dar es salaam wakiwa katika Kikao hicho.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.