• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA SIASA MOROGORO YARIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA SERIKALI, YATOA MAAGIZO

Posted on: September 27th, 2024

Kamati ya siasa ya Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro imeridhishwa na utendaji kazi wa Serikari ndani ya Mkoa huo katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa Mkoani humo.

Hayo yamebainishwa Septemba 27, mwaka huu na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro Bw. Joseph Masunga wakati wa ziara ya Kamati hiyo ya siku tano yenye lengo la kufanya tathmini ili kuona ubora wa miradi hiyo na hatua iliyofikiwa ukilinganisha na fedha zilizopokelewa (value for money).

Aidha, Bw. Masunga amesema, Serikali Kuu imefanya uwekezaji mkubwa kwa wananchi katika kutoa suluhisho la kiuchumi kwa kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa na mazao, kupata maji na matibabu kwa urahisi kazi hiyo inafanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka wananchi kulinda miundombinu ya umma ili idumu kwa muda mrefu likiwemo daraja la Luhembe Wilayani Kilosa.

"… niwaombe sana mshapata Daraja hili, naamini shughuli zenu zitaenda vizuri lakini mna hitaji kulitunza ili liweze kutumika kwa muda mrefu zaidi kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira hususan yanayozunguka Daraja …" amesema Bw. Joseph Masunga

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo amewataka wananchi kujitokeza kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura ili kuwa na haki ya kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliopangwa kufanyika Novemba 27, 2024 kwani amesema ni haki ya kila mtanzania kupiga kura ili kupata viongozi walio bora na watakaowaletea maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka wananchi kuacha kulima katika vyanzo vya maji kwani kufanya hivyo kunasababisha mito kubadili njia zao asilia, kuharibu miundombinu ikiwemo madaraja na Barabara badala yake amewataka kila mmoja kupanda miti ikiwemo minazi ili kuzuia mmomonyoko wa udongo na kujipatia nazi kwa matumizi ya nyumbani.

Sambamba na hayo, Mhe. Malima amekemea vikali wakulima wenye tabia ya kuchoma miwa kwa makusudi ili kupewa kipaumbele katika kuuza miwa hiyo na kusisitiza kushirikiana kuwafichua wakulima wenye tabia hiyo ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Nao wakazi wa Kijiji cha Kiberege Wilayani Kilombero akiwemo Bi. Rehema Kwanja wamefurahishwa na ujio wa kamati hiyo ya siasa huku wakiomba kuharakishwa kwa ujenzi wa majengo ya mama na mtoto ya hospitali ya Wilaya ya Kilombero ili kuepuka kufuata huduma hiyo mbali.

Siku ya kwanza kamati hiyo imeshatembelea miradi ya maendeleo katika Wilaya mbili za Kilosa na Kilombero, moja ya miradi hiyo ni Daraja la luhembe, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya ifakara Mji, Shule ya sekondari ya lipangalala, mradi wa maji na mradi wa Barabara ya Mkamba kwa kiwango cha lami.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.