• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA UKAGUZI RUWASA YATOA MAAGIZO.

Posted on: July 13th, 2022

Kamati ya Ukaguzi RUWASA yatoa maagizo.

Kamati ya Ukaguzi ya Wakala wa Usambazaji maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imeagiza kuharakishwa upatikanaji wa vifaa vya kuchuja maji katika mtambo wa Uzalishaji maji uliopo Wilayani Gairo ili mtambo huo uweze kurudi katika hali yake ya uzalishaji wa kawaida na kuwaondolea wananchi wa Gairo kero ya maji.


Mwenyekiti wa ufundi na Miradi (RUWASA) Mhandisi Ngwisa Mpembe akitoa maagizo kwa RUWASA Wilaya ya Gairo wakati wa ziara yake ya kukagua Miradi ya maji Julai 12 mwaka huu.


Meneja wa RUWASA Mkoa wa Morogoro Bw. John Msengi akizungumza wakati wa ziara hiyo.


Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa ufundi na Miradi (RUWASA) Mhandisi Ngwisa Mpembe Julai 12, 2022 wakati wa ziara ya Kamati hiyo ambayo imetembelea Miradi ya maji katika Wilaya za Gairo na Kilosa Mkoani Morogoro.


Wanakamati wa Bodi ya ufundi ya RUWASA wakiwa katika Kikao cha ndani wakati wa ziara ya kukagua miradi ya Maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Gairo.



Baada ya kutembelea Mtambo wa uzalishaji Maji Gairo Mjini Kamati hiyo imeshuhudia mtambo huo wenye uwezo wa kuzalisha lita milioni moja na laki nane kwa siku (1,800,000) ukiwa umeshuka kiwango cha uzalishaji wake kwa asilimia 50 kutokana na mashine moja kufanya kazi badala ya mbili.



“Mtambo huu unauwezo wa kuzalisha lita milioni moja na laki nane (1,800,000) kwa siku, lakini kwasababu za kiufundi sasa hivi uzalishaji umeshuka kwa karibia asilimia 50, kwa hiyo kama bodi tumeiagiza mamlaka chini ya usimamizi wa meneja wetu wa Mkoa kwanza kuharakisha kufanya kila liwezekanalo vifaa hivyo ambavyo ni membrane vifaa vya uchujaji vipatikane haraka”  amesema Mhandisi Mpembe.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji RUWASA Gairo Evance Mangosho amesema serikali imeshatenga bajeti ya Shilingi Milioni mia moja na hamsini {Tsh.150,000,000/=} kwa ajili ya ununuzi wa vifaa hivyo na wanatarajia mwezi wa tisa mwaka huu vifaa hivyo vitawasili kutatua tatizo hilo.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa RUWASA Gairo Evance Mangosho akiwaelekeza wanakamati wa RUWASA namna mitambo hiyo inavyofanya kazi.


 

Baadhi ya mitambo inayomilikiwa na RUWASA  Wilaya ya Gairo.

Naye Jumanne Raymond ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mapilipili B Wilayani Kilosa kwa niaba ya wananchi wake ameishukuru Serikali Pamoja na RUWASA kwa kuwaondolea changamoto ya maji katika eneo lake na kuwaomba kuendeleza usambazaji katika maeneo mengine ambayo haya japata Maji.



Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Mkoa wa Morogoro Mhandisi John Msengi amesema kuwa, wamepokea maelekezo yote yaliyotolewa na kamati hiyo kwa lengo la kuimarisha Zaidi upatikanaji wa maji safi na salama kwa Wananchi.



Miradi iliyotembelewa na Kamati hiyo katika wilaya hizo ni Mradi wa Mamlaka ya Maji Wilaya ya Gairo, Mradi wa jumuiya ya watumia Maji Berega Pamoja na Mradi wa maji Rudewa Wilayani Kilosa ambao inatekelezwa kwa fedha za UVIKO 19.





Baadhi ya wananchi wakifurahia huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama Wilayani Gairo na Kilosa.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.