• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kasi ya maambukizi ya UKIMWI yapungua kutoka 4.5% hadi 3.3%

Posted on: November 13th, 2024



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema kasi ya maambukizi mapya ya UKIMWI yamepungua kutoka asilimia 4.5 miaka sita iliyopita hadi asilimia 3.3 mwaka 2024 kutokana na juhudi kubwa za kamati ya afya inayoundwa na idara mbalimbali za afya na wadau mbalimbali wa Mkoa huo.

Mhe. Malima amesema hayo Novemba 13, Mwaka huu wakati akipokea msaada wa vifaa mbalimbali vya kutolea huduma katika sekta ya afya Mkoani Morogoro vyenye thamani ya Tsh. Mil. 52 aambavyo vimetolewa na shirika linaloshughulikia afya ya familia ya kimataifa (FHI 360) kwa kushirikiana na watu wa marekani (USAID) katika mradi wake (Epidemic Contro - EPIC) ukiwa na lengo la kupunguza na kuondoa maambukizi mapya ya UKIMWI hapa nchini.

Akifafanua zaidi, Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa maambukizi ya UKIMWI yaligundulika mwaka 1988 mpaka sasa ni zaidi ya miaka 36 na kwamba Elimu zinazotolewa kwa wananchi kuhusu ugonjwa huo imesaidia kutambua njia za kuzuia maambukizi mapya na walioambukizwa tayari wanapata usaidizi wa mapema kwa kupatiwa mahitaji muhimu ikiwemo dawa ili kuwa na afya bora.


“… kasi imepungua kutoka 4.5% hadi 3.3% sio ndogo kwani kuna kitu tunachofanya ambacho kipo sawa sawa ndio maana maambukizi yanashuka…” amesema Mhe. Adam Kighoma Malima.

Aidha, Mhe. Malima amesema kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia utafiti uliofanyika kuonesha kuwa mama mjamzito mwenye maambukizi ya ugonjwa huo kwa kuzingatia ushauri wa kitaalamu anaweza kujifungua mtoto asiye na maambukizi.

Kwa sababu hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wadau mbalimbali wa sekta ya afya Mkoani Morogoro kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya ugonjwa wa UKIMWI ili kufikia lengo la chini ya asilimia 2 au kuuondoa kabisa baada tathmini itakayofanyika tena miaka sita ijayo kwani kutokuwa na ugonjwa wa UKIMWI Mkoani humo inawezekana.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa huyo amelipongeza shirika hilo kwa kutoa misaada hiyo kwa sekta ya afya ili kuendelea kutoa huduma hiyo kwa haraka.

Kwa upande wake, meneja wa mradi wa EPIC Mkoa wa Morogoro Bw. Azizi Itaka amesema mradi huo unatoa huduma kwa Mikoa 11 ikiwemo Morogoro lengo likiwa na kudhibiti maambukizi mapya ya UKIMWI kwa kutekeleza afua tatu muhimu zikiwemo kutoa elimu ya kujikinga na virus vya UKIMWI, kutoa elimu ya mabadiliko ya tabia na kufanya upimaji wa ugonjwa huo na kufanya uchunguzi wa awali wa magonjwa ya ngono katika jamii na wakishagundulika kuathiriwa wanafanyiwa utaratibu wa kufika sehemu sahihi kwa ushauri na tiba kamili.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Best Magoma amelishukuru shirika hilo kwa kuona umuhimu wa kutoa msaada huo katika sekta ya afya ili kuongeza nguvu katika kuhudumia wananchi wanaopata maambukizi mapya ili kuwa na afya bora kama watu wengine.

Mradi wa EPIC ulianza 2020 – 2025 ukisimamiwa na serikali ya watu wa Marekali USAID ambapo wametoa vifaa mbalimbali vikiwemo makabati, mabegi, pamba, sindano, glovu za mikono, makoti, viatu na sanduku za kubebea vifaa mbalimbali kwa ajili ya kurahisisha utoaji wa huduma Mkoani Morogoro.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.