• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KATIBU MKUU KIJAZI ATETA NA VIONGOZI MOROGORO, ATOA MAAGIZO.

Posted on: June 4th, 2022

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Mandeleo ya Makazi Dk. Allan Kijazi ameuagiza Uongozi wa Mkoa wa Morogoro kufanya upya tathmini ya wadaiwa sugu wa mashamba makubwa Mkoani humo ili kuiwezesha Serikali kuchukua hatua stahiki kwa wamiliki wa mashamba hayo.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dr. Allan Kijazi akisikiliza na kutatua chcngamoto za watumishi wa Idara ya Ardhi Mkoa wa Morogoro, Juni 3 mwaka huu alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja.

Dk. Kijazi ametoa agizo hilo Juni 3 Mwaka huu wakati wa ziara yake ya Kikazi ya siku moja Mkoani humo ambayo pamoja na mambo mengine, ilikuwa na lengo la kusikiliza changamoto mbalimbali za watumishi wa Idara ya Ardhi pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa huo.


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu Anza-amen Ndossa akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dr. Allan Kijazi ili azungumze na Maafisa wa Idara ya Ardhi.



Katibu Mkuu katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Mkoa, ameweka wazi kuwa kitendo cha baadhi ya wamiliki wa mashamba makubwa kutolipa madeni ya kodi ya pango la umiliki wa ardhi ni kuikosesha Serikali mapato halali na hivyo kuisababishia Serikeli hasara.

“Kwanza tupate takwimu kamili ya madai ya mashamba yote makubwa kwa Mkoa wa Morogoro, madeni tunayowadai ili tuweze kuchukua hatua mahususi kuhusu wamiliki wa mashamba haya” amesema Dk. Kijazi.




Sambamba na hayo Dk. Kijazi ameonya utaratibu wa wananchi kuvamia mashamba na maeneo yaliyowazi au yasiyoendelezwa na baadae kuomba kupewa mashamba hayo ambapo baadhi ya wananchi huishia kuyauza maeneo hayo. amesema, utaratibu huo hautakuwa na tija katika Taifa na hivyo Serikali inalazimika kukemea tabia hiyo na kuchukua hatua kali ili kulinda ardhi kwa manufaa mapana ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.




Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Anza-amen Ndossa amemuomba Katibu Mkuu huyo kusimamia kikamilifu matumizi ya ardhi ya Mkoa huo kwani Mkoa wa Morogoro kiuchumi na kimaendeleo unategemea ardhi kwa zaidi ya 90% kupitia kilimo na ufugaji hivyo kuendelea kuwa na migogoro ya ardhi Mkoani humo ni chanzo cha kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi wa Mkoa huo na taifa kwa jumla.



Naye Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Mkoa wa Morogoro Frank Minzikuntwe amemuomba Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kibali cha kutoa hati miliki za kimila kwa kutumia mfumo wa zamani ili kupunguza au kumaliza kabisa migogoro ya ardhi iliyopo baina ya mtu na mtu au jamii na jamii Mkoani humo.


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Ally Machela ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuikopesha fedha Halmashauri hiyo kwa ajili ya zoezi la kupima viwanja katika maeneo ya Kata ya Kihonda upande wa Kiegea STAR CITY ili kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi kwa haraka ambapo hadi sasa zaidi ya viwanja 3600 vimepimwa kupitia mkopo huo.




Afisa Ardhi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Edward Lugakingira kwa niaba ya maafisa Ardhi wa Mkoa huo amebainisha kuwa bado kwa baadhi ya Halmashauri hazina Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya hali inayosababisha wananchi kufuata zaidi ya umbali wa 174Km kufuata huduma ya utatuzi migogoro ya ardhi katika Wilaya jirani hivyo kuongeza gharama kubwa kwa wananchi.





Katibu Mkuu Dr. Allan Kijazi akiwa katika picha ya pamojana watumishi wa idara ya ardhi Mkoani Morogoro baada ya kumalizika kwa mkutano wake na watumishi hao Juni 3 mwaka.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • RAIS MSTAAFU WA AFRIKA KUSINI AWATAKA WAAFRIKA KUENZI MASHUJAA WAO.

    May 23, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.