• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KATIBU MKUU WA OFISI YA MAKAMU WA RAIS AHIMIZA UPANDAJI MITI

Posted on: February 24th, 2022

KATIBU MKUU OFISI YA MAKAMU WA RAIS AHIMIZA UPANDAJI MITI

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mary Maganga ameitaka jamii kuwa na utamaduni wa kupanda miti katika maeneo yao na kutunza uoto wa asili ili kupunguza gesi joto (Hewa ukaa) inayosababishwa na ukataji miti na uharibifu wa misitu.

Katibu Mkuu Mary amesema hayo Februari 23 mwaka huu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi wa REDD+, hafla iliyofanyika Cate Hotel iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akifafanua zaidi Katibu Mkuu huyo amesema mradi huo una lengo la kuhifadhi uoto wa asili na misitu ambayo kwa sasa imeathiriwa na shughuli za kibinadamu na kupelekea hewa ukaa kuongezeka na kwamba suluhisho lake ni kupanda miti.

“Lakini wewe na mimi tukipanda miti katika maeneo yetu ya makazi, wewe na mimi tukitunza uoto wa asili tutaleta mabadiliko makubwa sana katika nchi yetu” amesema.

Aidha, amesema kikao hicho kinalenga kuzijengea uwezo zaidi taasisi mbalimbali za Serikali ambazo zinahusiana na masuala ya uhifadhi ili kuweza kutekeleza mradi huo kwa ufanisi zaidi yakiwemo mazingira ya Mkoa wa Morogoro ambayo uoto wake umeharibiwa sana.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mzingira Dkt. Andrew Komba, amesema zaidi ya hekta laki Nne za Misitu zinakatwa kwa mwaka hivyo kusababisha hewa ukaa kuongezeka hali ambayo amesema kama haitadhibitiwa italeta athari zaidi hapa nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya kuendeleza Kilimo katika Ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT) Geoffrey Kilenga amesema mradi huo unalenga kuendeleza kilimo rafiki yaani shughuli za uzalishaji hususan kilimo zinakuwa endelevu na zenye tija lakini bila kuharibu mazingira.

Mradi wa REDD+ kwa sehemu kubwa unafadhiriwa na Serikali ya Norway na ni moja ya jitihada za Serikali katika kushughulikia mabadiliko ya tabia nchi hivyo kupunguza madhara yake ikiwa ni pamoja na ongezeko la ukame, mafuriko ya mara kwa mara uhaba wa chakula na maji pamoja na kuyeyuka kwa seruji kwenye milima mirefu.

Imefahamika kuwa Mradi huo wa REDD+ hadi kukamilika kwake, utagharimu takribani dola za Marekani milioni mia tatu.



MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.