• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Katibu Tawala Msaidizi Biashara, Viwanda atoa maagizo

Posted on: September 6th, 2023

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji  Mkoani Morogoro Bi. Beatrice Njawa amewaagiza Wakuu wa idara ya viwanda, biashara na uwekezaji wa Halmashauri za Mkoa huo kugawa majukumu yao kwa Maafisa walio chini yao ili kutokwamisha utendaji kazi wa Serikali katika Halmashauri zao.

Bi. Beatrice ametoa wito huo kwa Maafisa hao Septemba 5 mwaka huu wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili cha kupeana uzoefu wa kiutendaji na kilichoshirikisha Wakuu wa Idara ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Morogoro.

Akihitimisha Kikao hicho kilichofunguliwa Agosti 4, 2023 na Katibu Tawala wa Mkoa huo Alhaji Dkt. Mussa Ali Mussa, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji amekitaka kikao hicho  kiwe na matokeo chanya hususan katika masuala ya Uwekezaji, Viwanda, Biashara na masoko.

Aidha, amewataka Viongozi wa ngazi hizo za Wilaya kuwasilisha taarifa zao za kazi zilizofanyika kwa mujibu wa Sheria, taratibu na kanuni za Kiserikali.

"... utekelezaji wa majukumu ni muhimu zaidi hivyo taarifa hizi ziwasilishwe kila baada ya robo mwaka na mnatakiwa kufanya mgawanyo wa majukumu kwani inawezekana mtu mmoja akawa anafanya vitu vingi wakati wengine wapo..." amesema Bi. Beatrice Njawa.

Aidha, amesema, pamoja na majukumu yao pia wanapaswa kufanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa ajili ya kuwasaidia wafanyabiashara hususan sekta binafsi na kuweza kufikia malengo ya serikali ya awamu ya sita ya inayoongoza na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wao, Maafisa biashara akiwemo Bw. Mohamed Kinuga kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi amesema kikao hicho kimewapa Elimu ambayo hawakuwa nayo kabla yake ikiwemo Elimu ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani, ambapo ameahidi kwenda kuwashawishi wakulima kutumia mfumo huo ili kujipatia bei inayoendana na thamani ya mazao wanayouza.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.