• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kikao cha mikakati, fedha za Uviko – 19 chaitishwa, RC ataka wataalamu kubaki vituoni, aagiza majengo kukamilika Disemba.

Posted on: October 18th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameitisha kikao cha dharura Mkoani humo kwa ajili ya kuweka mikakati ya matumizi ya fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO – 19 walizopata kutoka Serikalini.

Martine Shigela ameitisha kikao hicho Oktoba 17 mwaka huu kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa CCT Kilakala katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na kushirikisha wataalamu mbalimbali wa Halmashauri pamoja na Vyombo vya Ulinzi na Usalama ndani ya Mkoa huo.

Wakati wa ufunguzi, Martine Shigela amesema, kikao hicho sio cha kiitifaki bali ni kikao kinacholenga Mkoa kuweka mikakati ya kwenda mbele katika kutekeleza kwa ufanisi matumizi ya fedha zaidi ya Tsh. Tril. 1.3 alizotafuta Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika jitihada zake za Kupambana na Uviko – 19 na Mkoa kupata mgao wa zaidi ya Tsh. 19.9 Bil.

Kwa sababu hiyo, Mkuu wa Mkoa ameelekeza kwa sasa kuanza na ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa shule za Msingi na Sekondari ili  kutowakosesha wananfunzi masomo yao ifkiapo Januari mwakani na kuwataka kila Halmashauri kukamilisha majengo hayo ifikapo mwezi Disemba mwaka huu.

“Ningependa ikiwezekana kabla hata ya tarehe 15, tarehe mbili, tatu Nne ya Disemba tuanze kuona majengo ya madarasa ya wanafunzi wetu yamekamilika” ameagiza Shigela.

Pamoja na maagizo hayo amewataka Wakurugenzi pamoja na wataalamu wao kubaki vituoni kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa madarasa hayo kama walivyokubaliana kwenye kikao na kwamba hategemei kuona kiongozi wa Halmashauri kuondoka eneo lake la kazi kabla ya kukamilisha kazi hiyo.

“kama mimi Mkuu wa Mkoa siondoka, sitarajii mtu mwingine ataondoka kabla ya kukamilisha hii kazi, naomba sana, naongea kistarabu tena kwa kuwaomba, kipimo chetu ni kazi hii” amesisitiza Shigela.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa huo kutoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kila Ijumaa ya kila wiki na Oktoba 22 wawasilishe taarifa ya  kuwapata mafundi na taratibu za manunuzi wa vifaa vya ujenzi ili Mkoa uanze mchakato wa kuagiza vifaa  hivyo kiwandani kama walivyokubaliana kuwa manunuzi ya vifaa hivyo yatafanyika kwa pamoja kimkoa ili kupunguza gharama.

Hata hivyo Katibu Tawala wa Mkoa huo Bi. Mariam Mtunguja amefafanua suala la ununuzi wa vifaa vya ujenzi kuwa bado hilo ni jukumu la Wakurugenzi, katika kila hatua inayohitajika ya manunuzi kwa kufuata taratibu za manunuzi, Mkoa utahusika kwenye utaratibu pekee na kuhakikisha vifaa hivyo vinapatikana kwa gharama nafuu.

Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando yeye alishauri kuwa pamoja na uharaka na muda mfupi uliopo, ni muhim manunuzi hayo yasikiuke taratibu za kimanunuzi ili Mkoa usiweze kuingia kwenye mtego wa matumizi mabaya ya fedha wakati wa ukaguzi wa matumizi ya fedha hizo.

Huku Mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini Mhe. Innocent Kalogeresi ameshauri wataalamu katika ujenzi huo wa madarasa kujaribu kuona namna nyingine mbadala ya kupunguza gharama hususan katika matumizi ya matofali ya kuchoma.

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki Mhe. Hamis Tale Tale akiwasilisha taarifa kwa wajumbe wa  kikao hicho.

Aidha, wajumbe wengine wakiwemo wa Kamati ya Ulinzi na Usalama akiwemo mwakailishi wa Jeshi la Magereza Moa wa Morogoro, amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kuagiza kikao hicho kufanyika mapema huku akiwatoa wasiwasi wajumbe wa kikao hicho kuwa Jeshi la Magereza Mkoani humo lina uwezo wa kufanya kazi ya kujenga madarasa ndani ya Mkoa huo kwa ufanisi endapo litapewa ridhaa hiyo kama ilivyopendekezwa na wajumbe wa kikao hicho.



Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Morogoro waliohudhuria katika kikao hicho.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu, Mkoa wa Morogoro Bw. Anza Amen Ndosa alifafanua namna fedha zaidi ya Tsh. 19.9 Bil. zilizotolewa na Serikali zitakavyotumika Mkoani humo kuwa Tsh. 630,000,000/= zimelenga kujenga nyumba za watumishi, Tsh. 1.2Bil. zitatumika kununua X - ray na Tsh. 100Mil. Kujenga vyumba vya wagonjwa mahututi.

Katibu Tawala  wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja (kulia) akiteta neno na Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Mipango na Uratibu Anza Amen David Ndossa wakati wa kikao hicho.

Fedha nyingine ni Tsh. 900Mil. zitajenga majengo ya huduma za Dharura, Tsh. 80Mil. zitajenga miundombinu ya shule za wanafunzi wenye mahitaji maalum Wilayani Mvomero, Tsh. 2,840,000,000/= zitajenza vyumba vya madarasa katika vituo shikizi na Tsh.14,140,000,000/= zitajenga madarasa ya shule za Sekondari na kufanya jumla ya fedha zote Bil. 19,950,000,000/= kuwa zitatumika.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.