• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KINGA NI BORA KULIKO TIBA - DKT. MUSSA

Posted on: September 28th, 2024



Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amelishauri Shirika la Germany TB and Leprosy Relief Association ( GLRA) linalojishughulisha na ugonjwa wa ukoma, kujikita katika kutoa elimu ya namna ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo ili  kuzuia maambukiza mapya ya ukoma kwa jamii, kwa kuwa amesema KINGA NI BORA KULIKO TIBA.

Dkt. Mussa amesema hayo Septemba 26, 2024 wakati akizindua mpango wa  kutokomeza ugonjwa wa Ukoma Mkoa wa Morogoro, uzinduzi uliofanyika katika Hoteli ya Morena iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.



Amesema, programu mbalimbali zinazoanzishwa huwa hazizungumzii sana suala la kuzuia bali huzungumzia masuala ya kutibu hivyo amewataka wataalamu hao kuwa na mpango mkakati wa kuzuia kuenea kwa Ugonjwa huo wa ukoma.

".. kuna haja kwa sisi wataalamu tuendelee kusisitiza kutafuta mbinu  ya namna gani ya kuweza kufanya Prevention ya haya maradhi.."Amesisitiza Dkt. Mussa 

Aidha Dkt. Mussa amesema Mikoa ya Morogoro, Mtwara, Lindi, Tanga na visiwa vya Unguja ndio inasemekana ina visa vingi vya ugonjwa huo, hivyo amelitaka shirika hilo kuweka mkazo katika maeneo hayo ili kusaidia kujua chanzo cha kuenea kwa Ugonjwa huo.


Sambamba na hayo amelitaka Shirika hilo la GLRA kuwatumia wataalamu wa Afya walioko ngazi ya chini  kwa lengo la kutoa elimu ya jinsi ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wenyewe hivyo kusaidia kutoenea katika ngazi za chini.

Kwa upande wake Meneja wa Mpango wa Taifa wa TB na Ukoma Dkt. Liberate Mleoh amesema programu hiyo ni mahususi kwa ajili ya kutokomeza ugonjwa wa Ukoma lengo ni kwamba ifikapo 2023 kusiwe na maambukizi ya Ukoma.

Aidha, katika kikao hicho imebainishwa kuwa programu hiyo kwa Mkoa wa Morogoro inatekelezwa katika Wilaya tatu za Halmashauri  ya Mlimba, Ifakara Mji na Manispaa ya Morogoro, huku wito ukitolewa kwa Wananchi kutoa taarifa kwa wataalamu wa afya pindi mtu atapojihisi ana ugonjwa huo.


Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mlimba Dkt. Deodati  Jumanne akiongea kwa niaba ya waganga wa Halmashauri za Ifakara Mji na Halmashauri ya Manispaa amesema, mpango huo wameupokea na wapo tayari kuutekeleza ili kuzuia kuenea zaidi kwa ugonjwa huo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.