• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA 2025 ATOA MAAGIZO.

Posted on: April 12th, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Bw. Ismail Ali Ussi, ameutaka uongozi wa Wilaya ya Morogoro kuhakikisha unatatua changamoto zilizopo katika soko la chakula la Ngerengere ili wananchi wa Ngerengere na wengine wanaolitumia soko hilo waweze kufanya biashara zao ndani ya soko hilo bila bughudha yoyote.



Bw. Ussi ametoa agizo hilo Aprili 11, 2025, wakati akikagua soko hilo ikiwa ni siku ya kwanza ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Morogoro kwa ajili ya kuzindua, kuweka mawe ya msingi na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.



Amesema kuna umuhimu mkubwa kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Mussa Kilakala, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kushughulikia changamoto zote zinazolikabili soko hilo, zikiwemo miundombinu ya maji na vyoo, ili wafanyabiashara waweze kufanya kazi zao pasipo shida kwa maendeleo yao binafsi na ya taifa kwa ujumla.


“Kuna baadhi ya changamoto ambazo nimeziona katika soko hili; kabla hatujafika mkoa wa tano, marekebisho yafanyike na tupate taarifa,” amesema Bw. Ussi.


Aidha, amewataka wananchi wa Tarafa ya Ngerengere kutunza miundombinu iliyopo ndani ya soko hilo na kuitumia ipasavyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu, kwani serikali hutumia fedha nyingi kuijenga.


Katika hatua nyingine, Bw. Ussi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inalenga kuboresha maisha ya Watanzania katika sekta mbalimbali, ikiwemo sekta ya afya na upatikanaji wa maji vijijini.


Pia, ameishukuru jamii ya Kata ya Mikese kwa kuwakaribisha wawekezaji, hususan mwekezaji wa mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza nguzo za umeme za zege kitakachogharimu zaidi ya shilingi bilioni 3.5 hadi kukamilika kwake, na ambacho kinatarajiwa kutoa ajira kwa wananchi wapatao 120 wa tarafa hiyo.


Ameongeza kuwa kiwanda hicho kitasaidia kupunguza changamoto ya nguzo zinazodondoka, hali inayosababisha kukatika kwa umeme mara kwa mara, na kuwataka wananchi kukitunza kiwanda hicho kwa manufaa yao na vizazi vijavyo.


Mbio za Mwenge wa Uhuru mkoani Morogoro, katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, zimetembelea jumla ya miradi nane yenye thamani ya shilingi bilioni 4.4. Mwisho wa mbio hizo ulihudhuriwa na Bw. Ussi ambaye alifunga kongamano la vijana lililofanyika kwa siku saba na kujikita katika mafunzo ya uzalendo, maadili mema, na ujasiriamali.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.