• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kiongozi wa Mbio za Mwenge maalum wa Uhuru awataka watanzania kuipongeza Serikali

Posted on: August 9th, 2021

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru awataka watanzania kuipongeza Serikali

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Luteni Josephine Mwambashi amesema kuna kila sababu kwa watanzania kuishukuru Serikali yao na kuipongeza kwa namna inavyojali wananchi wake katika kuwapatia huduma muhimu kama Elimu, Afya na Maji.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Josephine Mwambashi

Luteni Mwambashi amesema hayo wakati wa Mwenge wa Uhuru ukipitia miradi ya maendeleo Wilayani Gairo ambapo pamoja na miradi mingine Mwenge wa uhuru uliona mradi wa maji wa Gairo ambao unagharimu zaidi ya Tsh 2 Bil.

“tuipongeze Serikali yetu kuona umuhim mkubwa kwa sisi wananchi kupata huduma hii ya maji kama ilivyosomwa katika taarifa kuwa huduma ya maji ilikuwa ni shida sana katika Wilaya hii ya Gairo” amesema.

Amesema kutokana na umuhimu wa maji Serikali ya awamu ya sita imesimamia mradi huo na kuona unakamilika kwa lengo la kuwaondolea kero wananchi wa Gairo hivyo hawana budi kuishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wakimbiza Mwenge kitaifa wakiwa juu ya tenki la maji kuhakiki utekelezaji wa mradi

Mtambo wa kuchuja maji ya chumvi katika mradi wa maji Gairo

Hata hivyo Luteni Mwambashi amepongeza mradi huo mkubwa unaotumia mtambo wa kisasa katika kuchunja kiwango kikubwa cha chumvi kinachofikia Micro siemens 6000 iliyoko kwenye maji hayo kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano - TEHAMA na kufanya maji hayo kuwa safi na salama kwa kunywa.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2021 amewataka wananchi pamoja na kutunza vyanzo vya maji lakini pia wanatakiwa kuwa walinzi wa miundombinu ya maji ili isiharibiwe na wapinga maendeleo hivyo kuendelea kupata maji karibu jambo litakalosaidia kupata muda wa kutosha kufanya shughuli nyingine za maendeleo.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabil Makame kwa niaba ya wananchi wa Gairo ameishukuru Serikali kukamilisha mradi huo na kuweka mtambo wa kuchuja maji huku akiahidi kuungana na wananchi wake katika kutunza vyanzo vya maji pamoja na miundombinu yake.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabil Makame akipokea Mwenge wa Uhuru 

Mwenge wa uhuru pamoja na miradi mingine sita umepitia mradi huo kwa lengo la kujionea namna unavyotumia TEHAMA katika kuchuja chumvi iliyoko kwenye maji yanayozalishwa hapo uku kiongozi wa mbio za Mwenge akikiri kuwa ameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo.

Mwenge wa Uhuru umekamilisha mbio zake Wilayani Gairo hii leo Agosti 9, 2021 na Agosti 10 utakimbizwa Wilaya ya Morogoro ikikamilisha idadi ya Wilaya saba za Mkoa wa Morogoro na Agosti 11  Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuanza kukimbizwa Mkoani Pwani.

Wakimbiza Mwenge kitaifa wakiwa katika picha ya pamoja na Bahati Msuliche wa Gairo (Mwenye ulemavu wa mikono) baada ya kumwona akiwa katika shughuli za mwenge kwa muda mrefu na mwenge kumzawadia fedha Tsh. 60,000/=

Baadhi ya Wakimbiza mwenge kimkoa wakiteta jambo. kushoto ni Wnnifrida Madeba Mratibu wa mbio za Mwenge  kimkoa - Morogoro


Baadhi ya wananfunzi wa shule za Msingi ambao wapo kwenye club za kupinga masuala ya Rushwa 

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.