• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2022 ATAKA USHIRIKIANO

Posted on: August 29th, 2022

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGEZA WA UHURU KITAIFA ATAKA WANANCHI KUSHIRIKIANA NA VYOMBO VYA USALAMA

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022 Sahili Geraruma amewataka wananchi wa Kiberege Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro na watanzania wote kwa jumla kutoa ushirikiano kwa vyombo vya Ulinzi na Usalama pale ambapo wanahitajika ili kujenga taifa la Tanzania linalosifika kama kisiwa cha Amani.



Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Hanji Godigodi (kushoto) akikabidhi risala ya Utii ya wananchi wa Wilaya hiyo kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2022 mara baada ya kusomwa na Katibu Tawala wake kwa niaba yake



Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Hanji Godigodi (kulia) akiwa katika picha ya makabidhiano ya Mwenge wa uhuru mara baada ya kuingia Wilayani kwake. kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Adam Bibangamba

Ndugu Sahili Geraruma ametoa kauli hiyo leo Agosti 29 wakati akifungua kituo cha Polisi cha Kata ya Kiberege Wilayani humo ambako Mwenge wa uhuru umekimbizwa kwa Km 183 na kupitia miradi sita yenye thamani ya zaidi ya shilingi 1.1 Bil.

Moja ya miradi iliyotembelewa na Mwenge wa Uhuru 2022

Akiwa katika Kituo cha Polisi cha Kata ya Kiberege Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amesema wananchi hawana budi kukitumia kituo hicho cha polisi kama kimbilio lao mara wanapopata matatizo yanayohusiana na polisi na kwamba wanatakiwa kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Polisi ili kudumisha Amani katika kata yao na Taifa kwa jumla.

“sambamba na hilo wanakiberege tuendelee kutoa ushirikiano kwa viongozi wetu hususan kwa askari Polisi, wapo kituoni hapa kuna jambo lolote unalolihisi hawa ndio usalama wako usisite fika, kuna ushahidi wako unahitajika njoo toa, ndio tunajenga Tanzania hii yenye Amani” amesema Ndugu Geraruma.  

Katika hatua nyingine kiongozi huyo wa mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa amewataka viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kufikiria kujenga nyumba za Askari polisi karibu na kituo hicho cha Polisi hao ili kurahisisha utendaji kazi wa askari polisi hao lakini pia kuwajengea mazingira mazuri ya kufanya kazi.

Amesema sio sahihi na haipendezi kabisa kukimbia au kutotoa ushahidi pale ambapo unapohitajika ikiwa ni pamoja na ushahidi unaohusu masuala ya ubakaji ili wale wanaotuhumiwa waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa amewataka askari polisi kutenda haki pale wanapopelekewa mashauri mbalimbali ya uvunjaji wa sheria, amesema wanatakiwa kuchukuliwa hatua wachukuliwe na asiyehusika aachiliwe huru aendelee na kazi ya kuijenga nchi yake.

Mwenge wa Uhuru kesho unatarajiwa kukimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi ikiwa ni Halmmashauri ya saba kati ya Halmashauri tisa za Mkoa wa Morogoro.



 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.