• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru ataka vyanzo vya maji kutunzwa.

Posted on: August 7th, 2021

Kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru Kitaifa  Luteni Josephine Paul Mwambashi amewataka wananchi wa Kijiji cha Miwangani Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro kutunza vyanzo vya maji ili kuondokana na kero ya maji waliyokuwa wakiipata hapo awali.

Luteni Josephine Mwambashi ametoa wito huo Agosti 7 mwaka huu wakati akizindua mradi wa maji uliopitiwa na Mwenge wa uhuru kukagua na kuridhishwa utekelezaji wake  wenye lengo la kuboresha miundo mbinu ya  mradi huo wa maji mserereko ambao ulisimamiwa na RUWASA wakishirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero (Mlimba) pamoja na wananchi.

Aidha, Kiongozi huyo wa mbio za mwenge amebainisha faida za kutunza chanzo vyanzo vya maji pamoja na miundombin yake hususan katika kijiji hicho kuwa ni kutosababisha maji ya mradi huo kukauka na hivyo kuwaondolea adha wananchi kufuata maji umbali mrefu zaidi.

Amesema, hapo awali akina mama na watoto walitumia muda mrefu kufuata maji mbali na kusababisha shughuli nyingine kusimama huku wanafunzi nao kutumwa kutafuta maji na kuacha masomo jambo ambalo liliwacheleweshea maendeleo yao.

“tunaendelea kusisitiza wananchi kutunza vyanzo vya maji kwa sababu mradi huu unatunufaisha sana kama tulivyosomewa kwenye taarifa, lakini uwepo wa mradi huu umesaidia sana akina mama na watoto kutumia muda waliokuwa wanafuata maji mbali kufanya shughuli nyingine…” amesema Luteni Josephine.


Kwa sababu hiyo amewataka wananchi wa Kijiji cha Miwangani kutunza chanzo cha maji cha mradi huo pamoja na miundombinu yake ili muda ule waliokuwa wanautumia awali kwenda umbali mrefu kutafuta maji sasa wautumie katika kujiletea maendeleo yao na ya taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Hanji Godigodi pamoja na Kuishukuru Serikali ya awmu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Kutoa fedha kwa ajili ya Mradi huo, ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wa Kijiji cha miwangani kwa kuunganisha nguvu zao na kuwezesha kuchimba mtalo wa kulaza mabomba umbali wa zaidi ya Km.6.4.


Awali Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kilombero Frolence Mlelwa akisoma taarifa ya Mradi huo mbele ya Kiongozi wa Mbio maaluma za Mwenge wa Uhuru amesema mradi huo ambao utatoa manufaa kwa wakazi wa Miwangani zaidi ya 2004 hadi kukamilika kwake umegharimu fedha za kitanzania 130,176,878.00.

Aidha, amesema kati ya kiasi hicho cha fedha, Tsh. 27,613,000.00 ni nguvu za wananchi zimetumika kupitia kuchimba mfereji kwa ajili ya kulaza mabomba ya maji ya mradi huo. 

Mwenge maalumu wa Uhuru  unaendelea na mbio zake Mkoani Morogoro ikiwa ni siku yake ya Nne tangu uanze kukimbizwa Mkoani humo na leo uko  Wilayani Kilombero ambapo umepitia miradi ya maendeleo saba ukiwemo mradi huo wa maji mserereko ambao umezinduliwa leo, Agosti 8 Mwenge wa uhuru utakimbizwa katika Wilaya ya Mvomero.

 

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.