• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA ATOA WIKI MOJA KUPATA HATI YA KIWANJA CHA MRADI.

Posted on: April 21st, 2024

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA ATOA WIKI MOJA KUPATA HATI YA KIWANJA CHA MRADI


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Godfley Mnzava ametoa wiki moja kwa  Halmashauri ya Wilaya ya Gairo kutafuta hati miliki ya kiwanja cha mradi wa upanuzi wa maji uliopo Kijiji cha Makuyu ili kuondoa changamoto zinazoweza kujitokeza  wakati mradi huo umeanza kutoa matunda na kunufaisha wananchi kama ulivokusudiwa wa kuondoa changamoto ya maji  kwa wananchi wa vijiji  lengwa


Kiongozi huyo wa Mbio Mwenge Kitaifa ametoa agizo hilo leo Aprili 21 wakati akizindua mradi wa upanuzi wa miundombinu ya maji katika Kijiji cha Makuyu unaolenga kuwanufaisha wananchi wa vijiji vya Kinyolisi na Iyogwe.

Aidha, ameagiza Wakala ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini -  RUWASA Pamoja na kuwa eneo hilo limetolewa na wananchi ili wapate maji bado wanatakiwa kufuatilia makubaliano hayo kuwekwa kimaandishi ili nyaraka hizo ziweze kusaidia mchakato mzima wa kuipata hati hiyo.  

Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Wilaya ya Gairo Mhandisi Gilbert Isac amesema mradi huo unakwenda sambamba na kauli mbiu ya kumtua mama ndoo kichwani huku akibainisha kuwa mradi huo unakwenda kunufaisha wananchi zaidi ya 6,000 hivyo kupunguza umbali mrefu waliokuwa wanaupata wananchi hao wa kutafuta maji.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Iyogwe ambaye ni mmoja wa Vijiji nufaika Bw. Richard Yeremia Kagoda, amesema kutokana na changamoto ya maji waliokuwa wanaipata siku za nyuma na baada ya kuona Serikali imekuja na mradi huo, waliamua kutoa eneo hilo bure kwa Serikali  ili mradi huo uweze kutekelezwa haraka.

Mradi huo unaogharimu Tsh. 513,050,359.33 bila VAT umelenga kusogeza huduma ya maji safi na salama kwa jamii ambao Fedha zake zimetolewa na serikali Kuu kupitia mpango wa  maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO – 19.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.