• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KITUO CHA AFYA MIKESE MKOANI MOROGORO KUANZA KUTOA HUDUMA.

Posted on: February 6th, 2023

 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI anayeshughulikia Afya Bi. Grace Magembe amemuagiza kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Bi. Ndelisho Moshi pamoja na Mganga Mfawidhi wa Halmashauri hiyo kuwa hadi kufikia Jumatatu ya wiki ijayo kituo cha Afya cha Mikese kianze kutoa huduma ya Afya Kwa wananchi wa Tarafa hiyo kutokana na kukamilika kwa miundombinu yote muhimu.

Naibu Katibu Mkuu huyo ametoa agizo hilo Februari 6 mwaka huu kwenye ziara yake iliyolenga kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho cha Afya na kujionea hali ya utoaji wa huduma za afya.

Aidha, Bi. Grace amesema ameridhishwa na ujenzi wa kituo hicho ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 100 suala lililobakia ni utoaji wa huduma Kwa wananchi na kuagiza kuwa Halmashauri ishughulikie suala la vifaa tiba pamoja na dawa ili wananchi wapate huduma mara moja.

“...Jumatatu huduma zianze kutolewa kwenye jengo hili...” ameagiza Bi. Grace Magembe.

Katibu Mkuu huyo ameeleza kuwa Serikali imetoa fedha  kiasi cha Shilingi million 400 Kwa ajili ya ujenzi wa majengo matano yakiwemo jengo la huduma ya mama na mtoto, Maabara, Wodi ya wazazi na jengo la dharura.

Sambamba na hilo, Naibu Katibu Mkuu huyo akiwa katika Zahanati ya Kijiji cha Fulwe amewahimiza wananchi kujiunga na bima ya afya iliyoboreshwa ili waweze kupunguza gharama za matibabu ambazo wanakutana nazo.

Kwa Upande wake Diwani wa Kata ya Mikese Mhe. Saidi Kimbeho ameeleza changamoto ya baadhi ya majengo na vifaa kuto tumika katika Zahanati ya Kijiji cha Fulwe na baadhi ya madaktari kuhamishwa hivyo kufanya baadhi ya huduma muhimu kama za maabara kukosekana.

Sambamba na changamoto hiyo bado amesema  gari la kubebea wagonjwa ni moja kwa Halmashauri nzima hivyo inaleta changamoto kwa wagonjwa wanaopata rufaa kwenda hospitali ya Mkoa kwa matibabu zaidi.

Nae Bi. Godliver Majige Mkazi wa Kata hiyo ya qMikese ameishukuru na kuipongeza Serikali pamoja na wahudumu wa Zahanati ya Fulwe kwa kuhakikisha kuwa huduma zinazotolewa kwa wananchi hao ni za uhakika na kutoa ombi kwa Naibu Katibu Mkuu huyo kuboresha huduma nyingine zikiwemo za maabara pamoja na kuongeza wahudumu wake ili kuleta ufanisi zaidi katika utoaji wa huduma hizo za afya.


Ziara hiyo ya Naibu Katibu Mkuu huyo ni utekelezaji wa agizo la Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Chongolo alilolitoa wakati wa ziara yake hivi karibu katika Wilaya hiyo kwa lengo la kuhakikisha kuwa huduma za afya zinaboreshwa na wananchi wananufaika mataibabu yanayotolewa.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.