• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kiwanda cha Sukari Kilombero chapongezwa kwa uzalishaji 26% ya sukari nchini.

Posted on: August 10th, 2023

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amewapongeza wawekezaji wa kiwanda cha sukari cha Kilombero ambacho kinazalisha asilimia 26 ya sukari inayotumiwa hapa nchini, na kuwataka kuweka mazingira mazuri kwa wakulima ili uzalishaji huo uongezeke.

Waziri wa Biashara na Viwanda Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akitoa maelekezo kwa uongozi wa kiwanda cha sukari cha Kilombero.

Waziri Kijaji ametoa pongezi hizo Agosti 10 mwaka huu alipotembelea kiwanda hicho kwa ajili ya kukagua hali ya uzalishaji wa sukari na maendeleo ya ujenzi wa kiwanda kipya cha sukari kinachoongezwa ikiwa ni  ziara yake ya siku mbili Mkoani Morogoro.

Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho wakipanga pakti za sukari iliyokuwa tayari ili kupelekwa sokoni.

Waziri huyo amesema nchi ina viwanda vikubwa zaidi ya vitano ambavyo vinazalisha sukari kikiwemo kiwanda cha sukari cha Kilombero, Mtibwa, Kagera, TPC - Moshi na Bagamoyo   lakini asilimia 26 ya sukari inazalishwa na kiwanda cha sukari cha Kilombero, hivyo ameupongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa uwekezaji wao na kazi nzuri wanayoifanya.

“…niwapongeze wawekezaji wa Kilombero sugar kwa kazi nzuri inayoendelea kufanyika…wao ni wazalishaji wa asilimia 26 ya sukari yote tunayotumia ndani ya nchi yetu…” amesema Waziri Kijaji.


Aidha, Waziri huyo amepongeza kazi kubwa ya ujenzi wa Kiwanda unaoendelea  kwa ajiri kuongeza ukubwa wa kiwanda hicho ambacho ujenzi wake unagharimu zaidi ya Tsh. Bilioni 500 na kwamba hiyo itasaidia wakulima wa miwa katika maeneo hayo hawatapata changamoto ya soko la miwa yao.

Katika hatua nyingine Waziri Kijaji amesema mwaka 2019 Serikali ilianzisha Mpango wa kuboresha Mazingira ya Uwekezaji na ufanyaji Biashara nchini (MKUMBI) mpango ambao umefanikiwa kwa asilimia 80 ambapo wawekezaji wengi wamefika nchini kuwekeza katika maeneo tofauti tofauti.

Aidha, Dkt. Kijaji amebainisha kuwa Serikali imefanya marekebisho ya sheria ya kodi ya mwaka 2023 ambayo imeanza kutumika tangu Julai 2023 kwa kuondoa na kufuta tozo na kodi ambazo zilikuwa ni miongoni mwa kikwazo cha wawekezaji na wafanyabiashara hapa nchini lengo ni kuvutia wawekezaji.

Waziri wa Biashara na Viwanda Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amepongeza mikakati iliyowekwa na uongozi wa kiwanda hicho kwa kuwapatia elimu wakulima kupitia maafisa ugani ambao wanachochea uzalishaji wa miwa wenye tija.


Aidha, amesema usajili wa wakulima kielektroniki unasaidia kuwatambua na kuwafikia wakulima  katika maeneo waliyopo.

Waziri Kijaji, RC Malima, DC Kyobya, uongozi na wataalamu mbalimbali wa kiwanda cha sukari cha Kilombero wakitembelea kiwanda hicho.

Naye, Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bw. Guy William amemshukuru Waziri wa Viwanda na Biashara ambapo amebainisha kuwa utanuzi wa kiwanda hicho utazalisha tani 271,000 za sukari na uzalisha huo utaondoa upungufu wa sukari nchini.

Mkurugenzi wa kiwanda cha sukari cha Kilombero Bw. Guy William akibainisha namna ya utendaji kazi baada ya kukamilisha upanuzi wa kiwanda hicho.

Hadi sasa ujenzi wa kiwanda hicho umefikia asilimia 60 na kinatarajia kuanza uzalishaji wake ifikapo Julai 2024.

Ziara ya Waziri Kijaji itaendelea Agosti 11, 2023 kwa kutembelea kiwanda cha Mkulazi kilichopo Mbigiri Wilayani Kilosa kuona maendeleo ya ujenzi huo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.