• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kiwanda cha sukari kilombero kuzalisha Tani 270,000 za sukari, RC Malima aridhishwa na ujenzi.

Posted on: July 23rd, 2023

Kiwanda cha Sukari cha Kilombero cha Mkoani Morogoro kinatazamiwa kuzalisha sukari tani 270,000 kwa mwaka mara kitakapokamilika ujenzi wake huku Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Malima akiridhishwa na ujenzi wa Kiwanda hicho kipya cha K4 unaoendelea.

Hapa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima anaangalia uzalishaji wa sukari katika kiwanda cha sasa kinachofanya kazi.

Hayo yamefahamika wakati wa ziara ya Mkuu huyo wa Mkoa wa Morogoro alipofanya ziara Julai 22 mwaka huu kwa lengo la kujionea upanuzi wa Kiwanda hicho huku akionesha kuridhihwa  na hatua iliyofikiwa.

Hili ni eneo ambalo kiwanda kipya cha sukari cha 4k kinajengwa.

Akiongea wakati wa ziara hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa ameweka bayana kuwa  kiwanda hicho cha kisasa kinachojulikana kama K4  kitakuwa na  uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 270,000 za sukari kwa mwaka.

Meneja wa kiwanda cha sukari cha kilombero Be. Guy William (wa tatu kushoto) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa Mhe. Adam Malima (wa pili kulia) wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Danstan Kiobya pamoja na kamati ya ulinzi na usalama.

"...kiwanda cha hapa Kilombero kitakuwa na uzalishaji wa tani 270,000, kile kiwanda cha miaka ya 60 cha zamani kinafungwa kwa hiyo tumepata bahati ya kwenda kukiona kinafanya kazi vizuri ila kinatumia nishati na gharama kubwa za uendeshaji" amesema Mhe. Malima.

Aidha, ameongeza kuwa kiwanda cha sasa kinatumia teknolojia ya miaka 60 iliyopita hivyo hutumia nishati na gharama kubwa kwa sababu hiyo kinapelekea kupanda kwa bei ya sukari, hata hivyo amebainisha kuwa kiwanda kinachojengwa sasa kitaleta ajira zaidi na unafuu kwa gharama ya sukari na gharama za uendeshaji wa Maisha kwa wananchi.

Mhe. Malima ameendelea kusema wawekezaji  wa kiwanda hicho wanapaswa kuweka mikakati na kutoa elimu kwa wakulima kwenda sambamba na kasi ya  uzalishaji wa kiwanda hicho cha kisasa ili wakulima hao wawe na uhakika na kulima mashamba makubwa huku kukiwa na uhakika wa masoko ya miwa inayolimwa.

Katika hatua nyingine Mhe. Malima ameipongeza serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na amani ambayo inayochochea uwekezaji mkubwa ukiwemo wa kiwanda hicho cha Sukari cha Kilombero huku akiwahakikishia wawekezaji wa kiwanda hicho usalama wa  uwekezaji wao.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wakiangalia  ujenzi wa kiwanda kipya cha sukari ambacho ujenzi wake unaendelea.

Lakini pia Mhe. Adam Malima amempongeza Meneja wa Kiwanda cha Sukari cha Kilombero (Kilombero sugar Company Limited) Guy William kwa kuonesha ushirikiano kwa Serikali hususan Katika kuchangia mapato ya nchi kwa kulipa ushuru unaostahiri kupitia Halmashauri za Ifakara Mji na Kilosa.

Naye, Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni  ya Sukari  ya Kilombero Bw. Fimbo Butara amesema bidhaa za sukari zina ubora ambao kila mwananchi anaweza kutumia kulingana na kipato chake kwani vipo vifungashio vya sukari hadi vya shilingi 200 hivyo amewataka wananchi kuendelea kutumia Sukari inayozalishwa Kiwandani hapo kwa sababu ina gharama nafuu na ina ubora unaohitajika.

Hapa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam Malima akiangalia mchakato wa uzalishaji sukari katika kiwanda cha sukari kilombero.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari Bw. Filbert Mpozi amesema hadi kufikia mwaka 2025 Tanzania haitaagiza sukari kutoka nchi za nje kutokana na kuwa na sukari ya kutosha hapa nchini hivyo amewapongeza wawekezaji wa kampuni hiyo ya uzalishaji Sukari ya Kilombero. 

Asilimia 75 ya kiwanda cha Sukari cha Kilombero kinamilikiwa na Illovo huku asilimia 25 ni Umiliki wa Serikali ya Tanzania na kina mchango mkubwa kwa jamii inayokizunguka kwa kutoa huduma za kijamii ikiwa ni pamoja na kutoa ajira kwa wananchi.

Kiwanda hicho hadi kukamilika kwake mwezi Julai mwakani kitagharimu Bil. 600 na kitazalisha  tani 270,000 kwa mwaka tofauti na sasa ambapo kinazalisha tani 130,000 pekee kwa mwaka.

Moja ya mtambo unaotumika kubeba miwa kwa ajili ya kuzalisha sukari kiwandani.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.