• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Kiwanda cha sukari Mkulazi kuondoa changamoto ya kuagiza tani 250,000 za sukari kutoka nje.

Posted on: August 11th, 2023


Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amekipongeza kiwanda kipya cha Sukari cha Mkulazi kwa mikakati iliyowekwa na wawekezaji wa kiwanda hicho ya kuzalisha tani zaidi ya 20,000 za sukari na kuondoa utegemezi wa kuagiza bidhaa hiyo nje ya nchi.

Waziri Kijaji amebainisha hayo Agosti 11 mwaka huu alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Mbigiri Wilayani Kilosa na kujionea maendeleo na hatua za ujenzi wake.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka katika kiwanda cha sukari Mkulazi.

Waziri huyo amesema Serikali huagiza tani 250,000 za sukari ya viwandani kwa mwaka hivyo, kiwanda hicho licha ya kuzalisha sukari ya matumizi ya majumbani lakini pia itazalisha sukari ili kulisha viwanda vinavyotumia mali ghafi hiyo.

“...kitu cha kupongeza katika kiwanda hiki ni kwamba kati ya viwanda vitano vikubwa tulivyonavyo hapa nchini hakuna hata kiwanda kimoja kinachozalisha sukari ya viwandani hivyo tunalazimika kuagiza sukari yote ya viwandani kutoka nje ya nchi...” amesema Waziri Kijaji.

Aidha, ameongeza kuwa Serikali imejenga kiwanda hicho na kufunga mifumo ya kuzalisha sukari hiyo ili ifikapo mwaka 2030 Serikali isiagize sukari kutoka nje.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuweka mazingira bora ya uwekezaji hususan Mkoani humo.

Aidha, amesema kiwanda cha sukari cha Mkulazi ni cha kimkakati kwa kuwa kitasaidia kupunguza matumizi ya fedha za kuagizia sukari nje ya nchi na kwamba kiwanda hicho kipya ni mfano kwa viwanda vingine.

Baadhi ya mitambo ya kuzalisha sukari katika kiwanda kipya cha sukari Mkulazi.

Naye, Mkurugenzi wa Udhibiti kutoka Bodi ya Sukari Bw. Lusomyo Buzingo amesema uzalishaji wa sukari unaotarajiwa kufanyika kiwandani hapo ni takribani tani 50,000 hadi tani 75,000 kwa mwaka utaongeza uzalishaji wa sukari kufikia tani 490,000 hivyo kupunguza uagizaji wa sukari kutoka nje na kupunguza matumizi ya pesa za kigeni.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiwa na Mhe. Adam Malima pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Mkulazi katika kikao kifupi cha kupokea taarifa ya kiwanda hicho.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.