• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Maadhimisho Siku ya UKIMWI Duniani 2023 kuzinduliwa Novemba 24, 2023 Morogoro.

Posted on: November 23rd, 2023

Kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani 2023 amabapo kitaifa Maadhimisho hayo yatafanyika Mkoani Morogoro huku Tarehe 24/11/2023 ni ufunguzi rasmi wa Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani 2023 na kufikia  kilelel tarehe 01 Disemba, 2023.  

Hayo yamebainishawa Novemba 23 mwaka huun na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam kighoma Malima wakati akizungumza kwenye Mkutano wa Waadishi wa Habari uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo uliolenga kutoa taarifa kuhusu Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani 2023 yatakayofanyika Mkoani humo.

Mhe. Malima amesema Wiki ya maadhimishoya siku ya UKIMWI Duniani itazinduliwa tarehe 24 Novemba, 2023 na kufikia kilele tarehe 01 Disemba, 2023. Katika wiki ya kuanzia tarehe 24 hadi 30 Novemba kutakuwa na mfululizo wa matukio na utoaji wa huduma mbalimbali zitakazotolewa na wataalamu zikiwemo upimaji wa VVU, uchunguzi wa magonjwa sugu yasiyoambukiza (Kisukari, Shinikizo la damu, uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa kizazi, lishe), elimu na uchunguzi wa Kifua Kikuu, uchangiaji damu na huduma ya kwanza. 

“...Katika wiki ya kuanzia tarehe 24 hadi 30 Novemba kutakuwa na mfululizo wa matukio na utoaji wa huduma mbalimbali zitakazotolewa na wataalamu zikiwemo upimaji wa VVU, uchunguzi wa magonjwa sugu yasiyoambukiza (Kisukari, Shinikizo la damu, Uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa kizazi, lishe), elimu na uchunguzi wa Kifua Kikuu, uchangiaji damu na huduma ya kwanza...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha matukio yatakayofanyika ndani ya Wiki ya Maadhimisho kuwa ni pamoja na  Mbio za nyika (ATF Marathon). Amesema Mbio hizo zinalenga kuhamasisha na kuutangaza mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI (ATF).

 Matukio mengine ni kufanyika kwa Kongamano la Vijana, kongamano la Kitaifa la Kisayansi (National HIV & AIDS Scientific Symposium),Mdahalo wa Viongozi wa Kijamii, tukio la Kilele cha Kijiji cha Vijana pamoja na Mkutano Maalumu wa Wadau wa Udhibiti UKIMWI (High level Partner’s meeting).

Sambamba na hilo Mhe. Adam Malima ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa huo, taasisi zote za Umma na Binafsi, Taasisi za Elimu ya vyuo vikuu na Jumuiya mbalimbali kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye maadhimisho hayo kuanzia siku ya ufunguzi tarehe 24 Novemba, 2023 hadi Disemba Mosi, 2023.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Watu waishio na Virusi vya UKIMWI (NACOPHA) Bw. Emanuel Msinga ameishukuru Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fursa kwa jamii hususan kwa watu waishio na VVU kuonesha mchango wao katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI. Aidha, ameishukuru Serikali kwa kutoa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI (ARV).

Mgeni rasmi siku ya kilele cha Maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.