• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MATUMIZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: January 28th, 2023

Bwana Vicent kayombo Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI akizungumza na Maafisa wa elimu wa Mikoa na Halmashauri nchini kwenye ufunguzi wa Mafunzo endelevu ya Walimu Kazini.

Maafisa elimu wa mikoa na Halmashauri hapa nchini wametakiwa kusimamia kwa usahihi fedha za miradi ya maendeleo hususan fedha zinazoendelezwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya shule yakiwemo madarasa kwa kuzingatia miongozo itakayotolewa na Serikali.

Agizo hilo limetolewa Januari 27, mwaka huu na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -  TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe kupitia hotuba yake iliyosomwa na Bwana Vicent Kayombo ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu wa TAMISEMI kwenye ufunguzi wa  kikao cha  usimamizi wa mafunzo endelevu ya walimu kazini (MEWAKA) kwa viongozi na waratibu wa MEWAKA ngazi za mikoa na Halmashauri,  uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha Uwalimu Mkoani Morogoro.

Akifafanua zaidi Bwana Vicent Kayombo amesema Muda si mrefu fedha za utekelezaji wa mradi wa BOOST zitatumwa Mikoani, Halmashauri, na shuleni ikiwemo fedha za ujenzi wa miundombinu ya shule hivyo wanatakiwa kuzisimamia fedha hizo kwa usahihi na kukamilisha miradi yote ya  ujenzi kwa wakati na kwa kuzingatia miongozo itakayotolewa na Serikali.

Aidha, Kayombo ameongeza kuwa zaidi ya Shilingi Bilioni 230 zitatumwa moja kwa moja shuleni, kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa, na Sekretarieti za Mikoa kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi hiyo.

"...Ni marufuku kutumia fedha au kutekeleza shughuli yoyote kinyume na miongozo ya miradi itakayotolewa". Kaimu Katibu huyo.

Sambamba na hilo, Bw. Kayombo kwa niaba ya  Katibu Mkuu TAMISEMI amewaagiza Maafisa elimu hao Kuimarisha usalama wa wanafunzi kwa kushirikiana na  jamii pamoja  na viongozi wa Serikali za Mitaa kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa iwekwe mifumo itakayowawezesha kuzuia na kubaini kama vitendo hivyo vinafanyika shuleni na kuchukua hatua stahiki  kwa mujibu wa sheria na miongozo iliyopo.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa BOOST Bw. Ally Swalehe amesema mafunzo hayo ni  sehemu ya utekelezaji wa sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014, mafunzo hayo yanahusisha jumla ya washiriki 286, wakiwemo maafisa elimu wa mikoa yote 26, maafisa elimu wa elimu ya awali na msingi kutoka Halmashauri 52, Wadhibiti ubora wa shule kutoka Halmashauri 52 na Waratibu wa Mafunzo endelevu ya walimu kazini kutoka halmashauri 52.

Nae Afisa Elimu Mkoa wa Morogoro Bi. Germana Mung’aho akitoa salam za Mkoa na kuwakaribisha wageni ndani ya Mkoa huo amesema wapo tayari kuyapokea mafunzo hayo na kwenda kuyafanyia kazi kwa manufaa ya walimu waliopo shuleni ili kuongeza ufanisi katika kazi zao.

Lengo kuu la MEWAKA ni kuimarisha utendaji wa walimu kwa kuwawezesha kukua kitaaluma ili kuboresha matokeo ya ufundishaji.

 Aidha, imeelezwa kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa sababu yatawawezesha walimu kupata mbinu mpya za kufundishia na kujifunzia, yataongeza motisha ya walimu kufanya kazi kwa kuwa watapata usaidizi wa kitaalamu kutoka kwa walimu wenzao, kuweka malengo yao ya kitaaluma yanayofikika, na kupata maarifa mbalimbali kuhusu masomo wanayofundisha.



MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • MAONESHO YA NANENANE July 27, 2022
  • View All

Habari Mpya

  • WAKULIMA WA MPUNGA KUNUFAIKA NA MRADI WA FTMA

    March 23, 2023
  • RAS MOROGORO AISHAURI TBA, AWATAKA KUFANYA KAZI KWA UFANISI

    March 21, 2023
  • TAASISI ZA KIDINI MOROGORO ZAPONGEZWA KATIKA KULETA MAENDELEO.

    March 20, 2023
  • SERIKALI YASHAURIWA KUTOA FEDHA KUTEKELEZA MIRADI YA UTAFITI

    March 16, 2023
  • View All

Video

Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.