• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MAAFISA TEHAMA MIKOA NA HALMASHAURI WANOLEWA KUHUSU MFUMO WA M-MAMA.

Posted on: June 16th, 2023

Katika juhudi za kukabiliana na vifo vya kinamama wajawazito na watoto wachanga hapa nchini Serikali inaendesha mafunzo ya mfumo wa usafirishaji wa dharura kwa mama mjamzito na mtoto yaani - M-mama yanayotolewa kwa wataalamu wa TEHAMA ngazi ya Mikoa na Hospitali za rufaa.

Mkurugenzi Idara ya TEHAMA Ofisi ya Rais -TAMISEMI Erick  Kitali wakati akifungua mafunzo ya usafirishaji wa dharura kwa mama mjamzito na mtoto M-MAMA.

Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika Queen Hotel katika Halmashauri ya  Manispaa ya Morogoro Mkurugenzi Idara ya TEHAMA Ofisi ya Rais -TAMISEMI Erick  Kitali amesema Pamoja na juhudi za Serikali, bado vifo vitokanavyo na uzazi vimeendelea kuwa juu.

Amesema, takwimu zinaonesha uwiano wa 578 kati ya vizazi hai 100,000 sawa na asilimia 18 ya vifo vyote vya wanawake wenye umri wa miaka 15-49.

Kitali amebainisha kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uelewa zaidi watalaam hao wa TEHAMA ili kukabiliana na changamoto za ucheleweshwaji unaosababisha matokeo mabaya ya uzazi kama vifo au ulemavu wa kudumu kwa wajawazito na watoto wachanga.

Mchambuzi wa Mifumo ya TEHEMA OR-TAMISEMI Shabani Zungiza amesema tayari Mikoa 16 imeshaanza kutumia mfumo huo wa M - Mama ambapo  sasa mgonjwa anaweza kupata huduma ya kupiga simu bure kupitia namba 115 ili kupata huduma hiyo.

“Tunafahamu tuna Changamoto kubwa hususani kwenye mifumo ya TEHAMA lakini maafisa TEHAMA ambao wapo ngazi ya Mikoa, Halmashauri na Hospitali za rufaa ni miongoni mwa watu ambao wanatakiwa kuhamasisha namna ya utumiaji wa mfumo huo” ameeleza Shabani Zungiza.

Kwa upande wake Afisa TEHAMA Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Ashura Sadiki amesema awali kulikuwa na changamoto kubwa ya mawasiliano lakini kupitia mfumo huo umerahisisha upatikanaji wa haraka wa huduma hiyo kwa akinamama wajawazito.

Pichani ni baadhi ya washiriki wa mafunzo ya usafirishaji wa dharura kwa mama mjamzito na mtoto M-MAMA wakiwa kwenye mafunzo hayo.

“ Mama mjamzito pamoja na mtoto ni watu ambao huwa mabadiliko yanatokea ghafla anaweza kupungukiwa damu ghafla au  mtoto anaweza kubadilika ghafla, kwa hiyo wanahitaji huduma hiyo ambayo ni ya haraka kwa hiyo Serikali imekuja na mfumo wa M-mama ambao unarahisisha mtoa huduma au anayehitaji huduma kupata huduma kwa haraka” amesema Ashura Sadiki.


Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.