• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Maafisa Ugani Morogoro watakiwa kuongeza jihudi, wapatiwa pikipiki.

Posted on: January 14th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amewaagiza Maafisa Ugani Mkoani humo kutumia muda wao mwingi kuwafundisha wakulima kwa vitendo namna bora ya kulima zao la mahindi  ili kuongeza uzalishaji  wenye tija katika zao hilo.

Loata Sanare amesema hayo Januari 13 mwaka huu Ofisini kwake  wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vyeti na zawadi za Pikipiki kwa Maafisa Ugani 10 kati ya 41 ambao wamefanya vizuri katika kuwafundisha wakulima namna bora ya  kulima na kuzalisha mahindi kwa ufanisi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo (kulia) akimkabidhi vyeti Mkuu  wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare kwa ajili ya kuwakabidhi Maafisa Ugani waliofanya vizuri katika kuwafundisha wakulima namna bora ya uzalishaji wa zao la mahindi.

Akiwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, Loata Sanare amesema kumfundisha mkulima uzoefu wa teknolojia bora ya uzalishaji wa mahindi kutoka nchini China kumesaidia kuongeza uzalishaji wa zao la mahindi kwa gharama ndogo, kuongeza upatikanaji wa chakula na kipato kwa wakulima.

 Aidha, Loata Sanare amesema mahindi ni zao la pili ambalo linalimwa kwa wingi baada ya mpunga katika Mkoa wa Morogoro hivyo  mradi huo ulikuwa chaguo bora linalogusa idadi kubwa ya wakulima katika Mkoa huo.

Kwa upande wake Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke amezungumzia namna Tanzania na China zinavyoshirikiana katika masuala ya kilimo katika mikoa mbalimbali hapa nchini ukiwemo Mkoa wa Morogoro ambako katika Mkoa huo kuna mashamba ya zao la Mkonge linaloendeshwa na China ambalo baada ya mkonge huo kuvunwa unasafirishwa nchini China ili kuliongezea thamani zao hilo.

Kuhusu mradi wa uzalishaji wa zao la mahindi kwa kutumia Teknolojia kutoka China  Balozi Wang Ke amesema mikoa mingine itaiga Mkoa wa Morogoro kutumia teknolojia kutoka China katika kuzalisha mahindi, uzalishaji utaongezeka kwa nchi nzima na hivyo wananchi wake watakuwa na uhakika wa chakula.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare akikabidhi vyeti kwa Maafisa Ugani waliofanya  vizuri katika kuwafundisha wakulima namna bora ya uzalishaji wa zao la mahindi

Naye, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Emmanuel Kalobelo amesema mradi wa kilimo cha mahindi baina ya China na Tanzania uliaza na vijiji viwili vya majaribio ambapo baada ya mafanikio viliongezeka vijiji  vingine kumi ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Morogoro lengo likiwa ni kuongeza  uzalishaji wa mahindi.

Akizungumzia mafanikio ya mradi huo Mhandisi Kalobelo, amesema hadi sasa wamefikia lengo la mradi la kuinua uzalishaji kutoka tani mbili kwa hekta hadi tani tatu kwa hekta.

Sambamba na hayo, Mhandisi Kalobelo amewataka Maafisa ugani kutumia pikipiki hizo kwa malengo yaliyokusudiwa ya kuwatembelea wakulima na kuwafundisha masuala ya kilimo huku akitahadharisha kuwa atakayebainika kukiuka matumizi ya pikipiki hizo atachukuliwa hatua kali za kinidhamu pamoja na kunyang’anywa pikipiki hiyo.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare akikabidhi pikipiki kwa Maafisa Ugani waliokidhi sifa za kupata zawadi hizo za pikipiki

Mdau mkubwa wa mradi huo Erenest Mkongo  amesema kabla ya maafisa ugani kupewa pikipiki hizo wakulima zaidi ya 2000 walifikiwa na Maafisa ugani hao, hivyo baada ya kupatiwa vyombo hivyo vya usafiri anatarajia idadi hiyo kuongezeka mara mbili zaidi

Mradi wa kilimo cha mahindi baina ya Tanzania na China ulianza mwaka 2013 kwa Vijiji 2 vya Pea Pea katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa na Mtego wa Simba katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kama vijiji vya mfano ambapo mwaka 2018 vikaanzishwa vijiji vingine 8 katika Halmashauri zote za Mkoa wa Morogoro na kufikia vijiji kumi.


MWISHO

                                                                         

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.