• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MAAFISA UGANI WAASWA KUONGEZA TIJA YA UZALISHAJI KWENYE KILIMO.

Posted on: March 27th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebecca Nsemwa amewataka Maafisa Ugani katika Mkoa wa Morogoro kuhakikisha kuwa wanaongeza tija ya uzalishaji kwenye kilimo kwani kwa sasa wamewezeshwa kuwafikia wakulima wengi zaidi hata wale walio maeneo yenye changamoto ya usafiri kwa kuwa Serikali imeowaondolea changamoto hiyo kwa kuwapatia pikipiki.

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa kauli hiyo Machi 27 mwaka huu kwenye  hafla fupi ya kukabidhi jumla ya Pikipiki 436 kwa Maafisa Ugani Mkoani Morogoro kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa, hafla iliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Ujenzi kilichopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Rebecca amesema anatarajia uzalishaji kwenye Sekta ya kilimo utaongezeka kwa sababu wataalamu hao wa kilimo wataweza kuwafikia wakulima kwa wakati na kutekeleza majukumu yao kwa wakati unaotakiwa.

"...tunauhakika uzalishaji wetu  katika maeneo yetu ya kilimo kwa sasa utakwenda kuimarika kwa sababu  wataalamu wetu  tunauhakika watakwenda kuwafikia au kumfikia mkulima mmoja mmoja..." amesema Mhe. Rebecca Nsemwa.

Ameongeza kuwa Pikipiki hizo 436 watapewa maafisa hao wa kila kata kwenye kila Halmashauri za Mkoa huo.

Aidha, ametumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake ya dhati ya kukuza sekta ya kilimo hapa nchini.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi upande wa Uchumi na Uzalishaji Dkt. Rozalia Rwegasira wakati akitoa taarifa fupi ya Pikipiki hizo, amesema Pikipiki hizo zimefungwa kifaa maalumu ambacho kinaonesha mahali ambapo Pikipiki hiyo ipo kwa wakati huo, hivyo amewataka Maafisa Ugani hao kuzitumia kwa ajili ya shughuli za kuwafikia wakulima kama ilivyoelekezwa na Wizara ya Kilimo.

Nae Bw. Wanted Mmari ambaye ni Afisa Ugani wa Manispaa ya Morogoro kwa niaba ya Maafisa Ugani wenzake amehaidi kuzitumia Pikipiki hizo kwa uaminifu kama walivyoelekezwa na Wizara ya kilimo.

Amesema kupitia usafiri huo utawasaidia kutekeleza majukumu yao kwa wakati, utafanya kuwafikia wakulima wengi zaidi katika maeneo yao.

Bi. Anna Msamo Afisa Ugani kata ya Mafisa ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka maafisa ugani hapa nchini.

 imeagizwa kuwa pikipiki hizo zitawasaidia Maafisa Ugani kupata takwimu sahihi za wakulima katika maeneo yao pamoja na kuwahudumia bila shida yoyote.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.