• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Maafisa wa Serikali wahimizwa kufuatilia Vituo vya kulelea watoto.

Posted on: February 28th, 2024

Maafisa Ustawi wa Jamii na Maendeleo jamii wametakiwa kuwa na utamaduni wa kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara kweye vituo vya kulelea watoto hususan katika vituo ambavyo havijasajiliwa ili viweze kusajiliwa na kuhakikisha vinafuata miongozo iliyotolewa na Wizara husika  namna ya kuendesha vituo hivyo.

Ushauri huo umetolewa Februari 28, 2024 na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu Mkoa wa Morogoro Bw. Anza Amen Ndosa wakati akifungua kikao cha mapitio ya utekelezaji wa program Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya watoto (PJT MMMAM) chenye lengo la kusimamia uratibu, ufuatiliaji na utekelezaji wa mpango wa huo katika ngazi mbalimabli kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chief Kingalu katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Bwana Ndosa ambaye katika tukio hilo amemwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa, amesema katika vituo hivyo vya kulelea watoto wadogo vihakikishe vinatoa malezi bora kwa kwao na maafisa hao wajenge utamaduni wa kuwatembelea mara kwa mara ili kujionea jinsi vituo hivyo vinavyotoa malezi yanayofaa kwa watanzania.

“…… Kwa hiyo niwaombe tena Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii kuhakikisha kwamba vituo vyote vya kulelea watoto wadogo vinasajiliwa na vinafuata miongozo iliyotolewa na Wizara ya Elimu katika kuviendesha vituo hivyo….” Amesema Bw. Ndosa.

Katika hatua nyingine Bw. Ndosa amewasisitiza Watendaji hao wa Serikali kushirikiana na viongozi wa dini katika kutoa elimu kwa jamii kupitia mikutano ya hadhara na vyombo vya habari juu ya  madhara ya unyanyasaji wa watoto na kuzingatia lishe bora kwa watoto ili waweze kukua vizuri na kuepuka athari ya upungufu wa lishe bora inayopelekea udumavu kwao.

Aidha, Katibu Tawala huyo ameishukuru Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali watoto kwa kuwajengea miundombinu ya Elimu kupitia mradi wa uboreshaji Elimu ya awali na msingi (BOOST) ambao unawasaidia kujifunza wakiwa katika umri mdogo na mazingira mazuri.

Kwa upande wake Mratibu wa Masuala ya Malezi na Ujifunzaji wa Awali kutoka Wizara ya Elimu Dkt. Hawa Juma Seleman amesema mtoto mdogo anatakiwa kupata huduma bora ikiwemo lishe, ujifunzaji wa awali na hatua za makuzi, Afya yenye uwiano na kwamba wadau wakizingatia hayo wataweza kutoa malezi yenye mwitikio chanya.

Naye Bi.Mary Shillah kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu –Idara ya Watoto, amewataka Watendaji hao wa Serikali kufanya kazi kwa umoja na ushirikiano ili kutoa malezi bora kwa watoto ambapo itasaidia kuondoa mmomonyoko wa maadili katika jamii zinazowazunguka.

Imeelezwa kuwa, Mkoa wa Morogoro una jumla ya vituo 263 vya kulelea watoto wadogo, kati ya hivyo vituo hivyo, vituo 85 pekee ndivyo vilivyosajiliwa kisheria.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.