• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Maagizo ya Waziri Mkuu yaaza kutekelezwa Morogoro.

Posted on: February 10th, 2021

Maagizo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kuhusu ufufuaji wa mashamba ya Mkonge yaliyotelekezwa na Kila Halmashauri kutenga angalau ekari 10 kwa ajili ya vitalu vya zao limeanza kutekelezwa Mkoani Morogoro.

Hayo yamebainishwa Leo Februari 10 mwaka huu baada ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare kuitisha kikao cha Wadaau wa zao la Mkonge kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo na kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wakulima na Uongozi Bodi ya zao la Mkonge Tanzania.

Loata Sanare amewaambia wadau hao kuwa Lengo la kikao hicho ni kuweka mikakati ya kutekeleza maagizo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano Tanzania aliyoyatoa Mkoani Tanga Januari 20, 2021 na kutaka kila Halmashauri ambazo zimetambulika kustawisha zao la Mkonge kufufua mashamba ya Mkonge huku akitaka halmashauri hizo kutenga japo ekari 10 kwa ajili ya kuandaa vitalu vya zao hilo na kuzigawa bure kwa wakulima.

Aidha, Loata Sanare amesema kikao hicho kitatoa taswira pana ya kuweka mpango kazi wa Mkoa katika kuliendeleza zao la Mkonge huku akitaka kila halmashauri inayolima zao hilo kufufua mazao ya mkonge yaliyotelekezwa, kuendeleza mashamba yanayolima na kuanzisha mashamba mengine mapya kwa ajili ya kustawisha zao hilo.

Maagizo mengine aliyoyatoa Mkuu huyo wa Mkoa ni pamoja na kutaka kuazishwa kwa vyama vya Ushirika vya mazao katika maeneo yanayolima zao hili ili kuwaunganisha wakulima wadogo wanaolima zao la Mkonge ili kurahisisha upatikanaji wa masoko na mitaji katika kukuza kilimo cha zao hilo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kufungua kikao hicho aliwaeleza wajumbe wa kikao hicho kuwa zao la Mkonge hapo awali lilikuwa linalimwa katika Halmashauri mbili tu za Kilosa na Morogoro.

Hata hivyo baada ya kufanyika uhamasishaji wa kutosha kutoka kwa Viongozi wa Serikalingazi ya Taifa, hivi sasa halmashauri za Gairo na Mvomero nazo zimeamua kulima zao hilo.

Aidha, Mhandisi Kalobelo amesema kwa sasa Mkoa una jumla ya mashamba sita yenye jumla ya ukubwa wa hekta 19,834 ambapo kati ya hizo hekta 7,573 zinalimwa sawa na 38% huku akiwatambulisha wakulima wadogo 14 wenye mashamba yenye ukubwa wa jumla ya hekta 245.

Mhandisi Kalobelo amebainisha shughuli zilizofanywa na Mkoa katika kutekeleza agizo la Serikali la kufufua zao la Mkoange, kuwa ni pamoja na kutambua mashamba yasiyoendelezwa mfano katika Wilaya ya Morogoro, jumla ya mashamba sita yenye ukubwa wa hekta 1,923 yamebainika na wamiliki wamepatiwa notisi ya siku 90 hadi februari 28, mwaka huu wawe wameonesha nia ya kuyaendeleza la, yatatwaliwa na kugawanywa kwa wananchi ili kulima zao la Mkonge.

Hatua nyingine iliyofanyika ni kutoa mafunzo kwa wataalamu wa kilimo, mafunzo yanayohusu kilimo cha mkonge ili waweze kutoa huduma ya ugani kwa wakulima kitaalamu zaidi, mafunzo hayo ya siku mbili yalitolewa na watafiti kutoka Mlingano na shughuli ya tatu ni uanzishwaji wa vitalu vya miche kupitia Halmashauri, mfano Halmashauri ya Gairo na Morogoro zimeazisha vitalu vya miche ya zao la Mkonge 32,000.

Nao wadau wa kikao hicho akiwemo cyriacus Faustine Ndyamkama kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha SUA alitaka vijana washirikishwe kikamilifu katika mkakati wa kufufua zao la Mkonge ili katika ushiriki wao waweze kupata faidika kutokana na kilimo cha zao hilo badala ya vijana wengi kwa sasa kuishia kufanya shughuli muda mfupi na hazina tija kubwa ikiwemo shughuli ya uuzaji wa laini za simu.

mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.