• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MADAKTARI WA DKT. SAMIA WAPONGEZWA MOROGORO.

Posted on: May 11th, 2024


Madaktari Bingwa zaidi ya 50 waliokuwa kwenye Kambi Maalum Mkoani Morogoro kwa ajili ya kutoa huduma ya matibabu kwa wananchi wamepongezwa kwa kufanya kazi kubwa na nzuri kwa siku tano tu walizofanya kazi hiyo.

Pongezi hizo zimetolewa Mei10 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa hafla fupi ya chakula cha pomoja kilichoandaliwa naye kwa ajili ya madaktari  hao wa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"... Nimehemewa,  nimefarijika sana kwa kazi nzuri mliyoifanya, ni jambo kubwa sana..." amesema Adam Malima.

Hata hivyo, Mhe. Malima amemshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaleta Madaktari hao Mkoani humo na kwamba jambo hilo ni kubwa na limeleta faraja kwa wananchi huku akitamani program hiyo kuendelea.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Pwani (Tumbi) Dkt. Aman Malima ambaye ni Mwenyekiti wa Kambi hiyo ya Kanda ya Kati, amesema lengo la awali katika program yao ni kuwaona wagonjwa 2000 hadi wanamaliza siku hizo tano wameweza kuwaona wagonjwa 3128.

Aidha, Dkt Aman aliyewawakilisha madaktari hao Bingwa wa Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoka Pwani, Dodoma, Singida, Iringa na wenyeji Morogoro amesema lengo la awali ni kufanya upasuaji wa wagonjwa100 lakini wameweza kufanya upasuaji wa wagonjwa 109 na wagonjwa wote wametoka salama.

Pamoja na na mafanikio hayo, Dkt Amani amesema Idara ikiyoongoza ni Idara ya magonjwa yasiyoambukizwa au magonjwa ya ndani yakiwemo magonjwa ya presha hivyo akatoa wito kwa jamii kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalam wa afya kuhusu lishe au ulaji wa vyakula pamoja na kufanya mazoezi.

Kambi ya Madaktari Bingwa Kanda ya kati imefanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kuanzia Mei 6 hadi 10, 2024 ikiwa ni azma ya Serikali ya awamu ya sita inaooyongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwasogezea wananchi huduma hiyo ya Afya karibu na wananchi ili kupunguza changamoto zao za kiafya.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.